< Isaiah 40 >

1 Comfort comfort people my he says God your.
Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Speak to [the] heart of Jerusalem and proclaim to it that it has been completed service its for it has been accepted iniquity its that it has received from [the] hand of Yahweh double for all sins its.
Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
3 A voice [is] calling in the wilderness make clear [the] way of Yahweh make straight in the desert plain a highway for God our.
Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
4 Every valley it will be lifted up and every mountain and hill they will become low and it will become the steep [place] level ground and the rough places a plain.
Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
5 And it will be revealed [the] glory of Yahweh and they will see [it] all flesh together for [the] mouth of Yahweh it has spoken.
Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
6 A voice [is] saying proclaim and he said what? will I proclaim all flesh [is] grass and all loyalty its [is] like [the] flower of the field.
Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
7 It dries up grass it withers a flower if [the] breath of Yahweh it blows on it truly [is] grass the people.
Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
8 It dries up grass it withers a flower and [the] word of God our it will stand for ever.
Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9 On a mountain high go up yourself O bearer of news of Zion lift up with strength voice your O bearer of news of Jerusalem lift [it] up may not you be afraid say to [the] cities of Judah here! God your.
Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
10 Here! [the] Lord Yahweh a strong [one] he will come and arm his [is] ruling for him here! reward his [is] with him and recompense his [is] before him.
Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
11 Like a shepherd flock his he will shepherd in arm[s] his he will gather lambs and in bosom his he will carry [them] nursing [ewes] he will lead.
Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
12 Who? has he measured in [the] hollow of hand his [the] waters and [the] heavens with span has he marked off? and has he contained? in third of a measure [the] dust of the earth and has he weighed? with balance mountains and hills with scales.
Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
13 Who? has he directed [the] spirit of Yahweh and [the] person of counsel his will he inform? him.
Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
14 With whom? did he take counsel and did he give understanding? him and did he teach? him [the] path of justice and did he teach? him knowledge and [the] way of understanding will he inform? him.
Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
15 There! nations like a drop from a bucket and like [the] dust of scales they are regarded there! islands like fine [dust] he lifts.
Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
16 And Lebanon not [is] sufficiency of burning and animal[s] its not [is] sufficiency of burnt offering.
Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
17 All the nations [are] as nothing before him from nothingness and emptiness they are regarded by him.
Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
18 And to whom? will you liken! God and what? likeness will you compare to him.
Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
19 The idol he has cast a craftsman and a metalsmith with gold he will overlay it and chains of silver [is] refining.
Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
20 The impoverished [person] a contribution wood [which] not it will rot he chooses a craftsman skillful he seeks for himself to prepare an idol [which] not it will be shaken.
Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
21 ¿ Not do you know ¿ not do you hear ¿ not has it been told from [the] beginning to you ¿ not have you understood [the] foundations of the earth.
Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
22 The [one who] sits above [the] circle of the earth and inhabitants its [are] like grasshoppers the [one who] stretched out like curtain [the] heavens and he spread out them like tent to dwell in.
Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
23 The [one who] appoints rulers to nothing judges of [the] earth like nothingness he makes.
Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
24 Even not they have been planted even not they have been sown even not it has taken root in the ground rootstock their and also he blows on them and they have dried up and a tempest like chaff it carries off them.
Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
25 And to whom? will you liken me and I may be equal? he says [the] holy [one].
“Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
26 Lift up height eyes your and see who? did he create these the [one who] brings out by number host their all of them by name he calls from greatness of strength and a strong [one] of power any not it is missing.
Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
27 Why? do you say O Jacob so you may declare? O Israel it is hidden way my from Yahweh and from God my justice my it passes away.
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
28 ¿ Not do you know or? not have you heard [is] a God of perpetuity - Yahweh [the one who] created [the] ends of the earth not he grows weary and not he becomes weary there not [is] inquiry to understanding his.
Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
29 [he is] giving To the weary [person] strength and to [those who] there not [is] power strength he increases.
Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
30 And they may grow weary youths so they may become weary and young men certainly they stumble.
Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
31 And [those who] wait for Yahweh they will renew strength they will go up wing[s] like eagles they will run and not they will become weary they will walk and not they will grow weary.
bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

< Isaiah 40 >