< Isaiah 25 >

1 O Yahweh [are] God my you I will exalt you I will give thanks to name your for you have done wonder[s] plans from distant [time] faithfulness faithfulness.
Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
2 For you have made from a city into heap a town fortified into a ruin a fortress of strangers from a city for ever not it will be rebuilt.
Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
3 There-fore they will honor you a people strong a town of nations ruthless they will fear you.
Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.
4 For you have been a refuge for the poor [person] a refuge for the needy [person] when it was distress to him a shelter from rainstorm a shade from heat for [the] breath of ruthless [people] [is] like a rainstorm of a wall.
Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
5 Like heat in a dry land [the] uproar of strangers you will subdue heat in [the] shade of a cloud [the] song of ruthless [people] he will quieten.
na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
6 And he will make Yahweh of hosts for all the peoples on the mountain this a feast of fat things a feast of old wine fat things full of marrow old wine refined.
Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
7 And he will swallow up on the mountain this [the] surface of the covering - which covers over all the peoples and the woven stuff which is woven over all the nations.
Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
8 He will swallow up death to perpetuity and he will wipe away [the] Lord Yahweh tear[s] from on every face and [the] reproach of people his he will remove from on all the earth for Yahweh he has spoken.
yeye atameza mauti milele. Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Bwana amesema hili.
9 And someone will say in the day that here! [is] God our this we have waited for him and he will save us this [is] Yahweh we have waited for him let us be glad and let us rejoice in salvation his.
Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
10 For it will rest [the] hand of Yahweh on the mountain this and it will be trampled down Moab in place its as is trampled down a heap of straw (in *Q(K)*) a dung hill.
Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
11 And it will spread out hands its in midst its just as he spreads [them] out swimmer to swim and he will bring low haughtiness its with [the] tricks of hands its.
Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
12 And [the] fortification of [the] refuge of walls your he will lay low he will bring [it] low he will make [it] touch the ground to [the] dust.
Atabomoa kuta ndefu za maboma yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

< Isaiah 25 >