< Hebrews 6 >
1 Therefore having left the beginning of Christ [of the] teaching to maturity we may go on not again a foundation laying of repentance from dead works and faith in God,
Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tukisonga mbele ili tufikie utimilifu, sio kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,
2 about baptisms (about teaching, *NK(o)*) about laying on then of hands, about [the] resurrection both of [the] dead and about judgment eternal. (aiōnios )
mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios )
3 And this (we will do *NK(o)*) if indeed if indeed shall permit God.
Mungu akitujalia tutafanya hivyo.
4 [It is] impossible for to those once having been enlightened, having tasted then of the gift heavenly and partakers having become of [the] Spirit Holy
Kwa kuwa ni vigumu kwa wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu,
5 and [the] goodness having tasted of God’s declaration [the] power also [of the] coming age — (aiōn )
ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao, (aiōn )
6 and then having fallen away — again to restore [them] to repentance crucifying in themselves the Son of God and subjecting [Him] to open shame.
kisha wakianguka, kuwarejesha tena katika toba. Kwa kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili na kumdhalilisha hadharani, nayo ikawa hasara kwao.
7 Land for having drunk in the upon it coming often rain and producing vegetation useful for those for the sake of whom also it is tilled, partakes of blessing from God;
Ardhi ile ipokeayo mvua inyeshayo juu yake mara kwa mara hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao kwa ajili yao yalimwa, nayo nchi hiyo hupokea baraka kutoka kwa Mungu.
8 [That] bringing forth however thorns and thistles [is] worthless and a curse near to, of which the end [is] unto burning.
Lakini ardhi ikizaa miiba na mibaruti, haina thamani na iko hatarini ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.
9 We have been persuaded however concerning you, beloved, [of] [things] better and [things] accompanying salvation, if even like this we speak.
Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu wapendwa, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mema zaidi, mambo yale yahusuyo wokovu.
10 Not for unjust [is] God to forget the work of you and (the labor *K*) the love that you have shown toward the name of Him having ministered to the saints and [still] ministering.
Mungu si mdhalimu: yeye hataisahau kazi yenu na upendo ule mlioonyesha kwa ajili yake katika kuwahudumia watakatifu na hata sasa mnaendelea kuwahudumia.
11 We desire now each of you the same to show earnestness toward the full assurance of the hope unto [the] end;
Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho,
12 so that not sluggish you may be, imitators however of those through faith and patience inheriting the promises.
ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.
13 For to Abraham having made His promise God, since by no [one] He had greater to swear, He swore by Himself
Mungu alipompa Abrahamu ahadi yake, kwa kuwa hakuwepo mwingine aliyekuwa mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake, aliapa kwa nafsi yake,
14 saying; (If *N(k)O*) surely blessing I will bless you and multiplying I will multiply you;
akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”
15 And thus having waited patiently he obtained the promise.
Abrahamu naye, baada ya kungoja kwa saburi, alipokea kile kilichoahidiwa.
16 Men (indeed *k*) for by [one] greater swear, and in all their disputes finally [comes] to confirmation in the oath;
Wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuwaliko, nacho kiapo hicho huthibitisha kile kilichosemwa na hivyo humaliza mabishano yote.
17 In which more excessive desiring God to show to the heirs of the promise the unchangeableness of the purpose of Him guaranteed [it] by an oath,
Mungu alipotaka kuonyesha kwa udhahiri zaidi ile asili ya kutokubadilika kwa ahadi yake kwa warithi wa ahadi, aliithitibisha kwa kiapo.
18 so that through two things unchangeable, in which [it is] impossible to lie (*n*) [for] God, strong encouragement we may have having fled for refuge to take hold of what is being set before [us] hope;
Mungu alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyobadilika, yaani ahadi yake na kiapo chake, ambavyo kwavyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi ambao tumemkimbilia ili tulishike lile tumaini lililowekwa mbele yetu tuwe na faraja thabiti.
19 which as an anchor we have of the soul sure both and unshakable and entering into that within the veil,
Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho iliyo imara na thabiti. Tumaini hili huingia katika sehemu takatifu iliyopo nyuma ya pazia,
20 where [the] forerunner for us has entered Jesus according to the order of Melchizedek a high priest having become to the age. (aiōn )
mahali ambapo Yesu mtangulizi wetu aliingia kwa niaba yetu. Yeye amekuwa Kuhani Mkuu milele, kwa mfano wa Melkizedeki. (aiōn )