< Hebrews 2 >
1 Because of this it behooves more abundantly to give heed us to the [things] we have heard, otherwise otherwise (we may drift away. *N(k)O*)
Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.
2 If for the through angels having been spoken word was unalterable, and every transgression and disobedience received a just recompense,
Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,
3 how we ourselves will escape such a great having neglected a salvation? which a commencement having received declaring through the Lord by those having heard to us it was confirmed
je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.
4 bearing witness God by signs together with [them] and by wonders and by various miracles and of [the] Spirit Holy by distributions according to the of Him will.
Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.
5 Not for to angels did He subject the world which is coming concerning which we are speaking;
Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika.
6 Has testified however somewhere someone saying; What is man that You are mindful of him or [the] son of man that You care for him?
Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema: “Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
7 You made lower him a little some than [the] angels; with glory and with honor You crowned him (and you appointed him upon the works of hands of you; *KO*)
Umemfanya chini kidogo kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8 all things You have put in subjection under the feet of him. In for subjecting to him all things no [thing] He left to him unsubject; At present however not yet do we see to Him all things subjected.
nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake.
9 Who however a little one than [the] angels made lower we see Jesus because of the suffering of death with glory and with honor crowned, so that (by [the] grace *NK(O)*) of God for everyone He may taste death.
Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.
10 It was fitting for to Him, for whom [are] all things and through whom [are] all things, many sons to glory having brought, the archetype of the salvation of them through sufferings to make perfect.
Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
11 The [One] both for sanctifying and those being sanctified of one [are] all; for which reason not He is ashamed brothers them to call
Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake.
12 saying: I will declare the name of You to the brothers of Mine, in [the] midst of [the] congregation I will sing praises of you.
Yeye husema, “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”
13 And again: I myself will be already trusting in Him. And again: Behold I myself and the children whom to Me has given God.
Tena, “Nitaweka tumaini langu kwake.” Tena anasema, “Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”
14 Since therefore the children have partaken of blood and of flesh also He himself likewise took part in the same things, so that through [His] death He may destroy the [one] the power holding of death, That is the devil,
Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi,
15 and may set free those as many as fear of death through all [times] of them to live subject they were to slavery.
na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.
16 Not for surely somewhere surely somewhere [the] angels He helps, but [the] seed of Abraham He helps.
Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu.
17 Therefore it was necessary in all things [His] brothers to be made like, so that a merciful He may become and faithful high priest [in] [things] relating to God in order to make propitiation for the sins of the people.
Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu.
18 In that for has suffered He Himself having been tempted, He is able those being tempted to help.
Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.