< Hebrews 11 >
1 Is now faith of [things] hoped for [the] assurance, of things [the] conviction not being seen.
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
2 In this for were commended the ancients.
Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
3 By faith we understand to have been formed the ages by declaration of God so that which not out of [things] being visible (the [thing] being seen *N(k)O*) becoming. (aiōn )
Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn )
4 By faith a more excellent sacrifice Abel than Cain offered to God, through which he was testified to be righteous bearing witness to the gifts of him (God; *NK(o)*) and through it having died still (he speaks. *N(k)O*)
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
5 By faith Enoch was translated not to see death and not was he found because took up him God; Before for the translation (of him *k*) he has been commended to have pleased God;
Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
6 Without now faith [it is] impossible to please [Him]; To believe for it behooves the one drawing near to God that He exists and [that] to those earnestly seeking out Him a rewarder He becomes.
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
7 By faith having been divinely instructed Noah concerning the [things] not yet seen having been moved with fear he prepared an ark for [the] salvation of the household of him, through which he condemned the world and of the according to faith righteousness [that is] he became heir.
Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
8 By faith (the [one] *o*) being called Abraham obeyed to go out into (*k*) a place that he was going to receive for an inheritance and went out not knowing where he is going.
Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
9 By faith he sojourned in (the *k*) land of the promise as [in] a foreign [country] in tents having dwelt with Isaac and Jacob the joint-heirs of the promise same;
Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
10 He was awaiting for the foundations having city of which [the] architect and builder [is] God.
Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
11 By faith also herself Sarah ([being] barren *N*) power for [the] conception of seed received even beyond [the] opportune age (she brought forth *K*) since faithful she considered the [One] having promised.
Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
12 Therefore also from one man were born, and he as good as dead, even as the stars of heaven in multitude and (as *N(k)O*) the sand by the shore of the sea countless.
Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
13 In faith died these all not (having received *NK(O)*) the promises but from afar them having seen and (having been persuaded and *K*) having embraced [them] and having confessed that strangers and sojourners they are on the earth.
Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
14 Those for such things saying make manifest that their country they are seeking.
Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
15 And if indeed that [one] (they were remembering *NK(o)*) from where (they came out, *N(k)O*) they had then would opportunity to return;
Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 (now *N(k)O*) however to a better [one] they stretch forward to, That is to a heavenly [one]; Therefore not is ashamed of them God God to be called of them; He has prepared indeed for them a city.
Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
17 By faith has offered up Abraham Isaac Being tested, even [his] only begotten [son] was offering up the [one] the promises having received,
Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
18 as to whom it was said that In Isaac will be reckoned your offspring;
Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
19 having reasoned that even out from [the] dead to raise able [was] God, from where him also in a simile he received.
Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
20 By faith (also *no*) concerning [the things] coming blessed Isaac Jacob and Esau.
Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
21 By faith Jacob dying each of the sons of Joseph blessed and worshiped on the top of the staff of him.
Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
22 By faith Joseph dying concerning the exodus of the sons of Israel made mention and concerning the bones of him gave instructions.
Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
23 By faith Moses having been born he was hidden three months by the parents of him because they saw [was] beautiful the little child and not they did fear the edict of the king.
Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 By faith Moses grown having become he refused to be named [the] son of [the] daughter of Pharaoh,
Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 rather having chosen to suffer affliction with the people of God than [the] temporary to have of sin enjoyment;
Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
26 greater wealth having esteemed than that (in *k*) (Egypt *N(k)O*) treasures the reproach of Christ; he was looking for toward the reward.
Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
27 By faith he left Egypt not having feared the anger of the king; the for Invisible [One] as seeing he persevered.
Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
28 By faith he has kept the Passover and the sprinkling of the blood, so that not the [one] destroying the firstborn may touch them.
Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
29 By faith they passed through the Red Sea as through dry (land, *no*) which an attempt having made the Egyptians were swallowed up.
Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
30 By faith the walls of Jericho (fell *N(k)O*) having been encircled for seven days.
Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
31 By faith Rahab the prostitute not did perish with those having disobeyed having received the spies with peace.
Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 And what more shall I say? Will fail me for telling the time of Gideon, Barak, (both and *k*) Samson, (and *k*) Jephthah, David also and Samuel and the prophets;
Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
33 who through faith conquered kingdoms, administered justice, obtained promises, shut [the] mouths of lions,
ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
34 quenched [the] power of fire, escaped [the] blades of [the] sword, (be empowered *N(k)O*) out of weakness, became mighty in war, [the] armies put to flight of foreigners.
wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
35 Received back women by resurrection the dead of them; others then were tortured not having accepted release, so that a better resurrection they may obtain;
Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
36 Others then of mockings and of scourgings trial received, in addition also of chains and imprisonment;
Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
37 They were stoned, they were sawed in two (tested *KO*) by slaughter of [the] sword they were killed; they wandered in sheepskins, in goats’ skins, being destitute, being oppressed, being mistreated,
Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
38 of whom not was worthy the world; (in *N(k)O*) deserts wandering and in mountains and in caves and in the holes of the earth.
watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
39 And these all having been commended through the faith not did receive the promise
Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
40 God for us better something having planned, so that not apart from us they may be made perfect.
Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.