< Genesis 37 >

1 And he dwelt Jacob in [the] land of [the] sojournings of father his in [the] land of Canaan.
Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
2 These - [are] [the] accounts of Jacob Joseph [was] a son of seven-teen year[s] he was shepherding with brothers his the flock and he [was] a youth with [the] sons of Bilhah and with [the] sons of Zilpah [the] wives of father his and he brought Joseph report their bad to father their.
Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
3 And Israel he loved Joseph more than all sons his for [was] a son of old age he for him and he made for him a long garment of palms and soles.
Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
4 And they saw brothers his that him he loved father their more than all brothers his and they hated him and not they were able to speak to him to welfare.
Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
5 And he dreamed Joseph a dream and he told [it] to brothers his and they increased again to hate him.
Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
6 And he said to them hear please the dream this which I have dreamed.
Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
7 And there! we [were] binding sheaves in [the] middle of the field and there! it arose sheaf my and also it stood upright and there! they gathered round sheaves your and they bowed down to sheaf my.
Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
8 And they said to him brothers his ¿ really will you reign over us or? certainly will you rule over us and they increased again to hate him on dreams his and on words his.
Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
9 And he dreamed again a dream another and he recounted it to brothers his and he said here! I have dreamed a dream again and there! the sun and the moon and one [plus] ten stars [were] bowing down to me.
Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
10 And he recounted [it] to father his and to brothers his and he rebuked him father his and he said to him what? [is] the dream this which you have dreamed ¿ really will we come I and mother your and brothers your to bow down to you [the] ground towards.
Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
11 And they were jealous of him brothers his and father his he kept the matter.
Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
12 And they went brothers his to pasture [the] flock of father their at Shechem.
Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
13 And he said Israel to Joseph ¿ not [are] brothers your pasturing at Shechem come! and I will send you to them and he said to him here [am] I.
naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
14 And he said to him go please see [the] welfare of brothers your and [the] welfare of the flock and bring to me word and he sent him from [the] valley of Hebron and he came Shechem towards.
Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
15 And he found him a man and there! [he was] wandering in the open country and he asked him the man saying what? are you seeking.
mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
16 And he said brothers my I [am] seeking tell! please to me where? [are] they pasturing.
Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
17 And he said the man they have departed from here for I heard [them] saying let us go Dothan towards and he went Joseph after brothers his and he found them at Dothan.
Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
18 And they saw him from a distance and just before he drew near to them and they dealt deceptively with him to kill him.
Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
19 And they said each to brother his there! [the] master of dreams this [is] coming.
Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
20 And now - come and let us kill him and let us throw him in one of the pits and we will say an animal wild it has eaten him and we may see what? will be dreams his.
Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
21 And he heard Reuben and he rescued him from hand their and he said not let us strike him life.
Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
22 And he said to them - Reuben may not you shed blood throw him into the pit this which [is] in the wilderness and a hand may not you stretch out on him so as to rescue him from hand their to restore him to father his.
Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
23 And it was just when he came Joseph to brothers his and they stripped Joseph long garment his [the] long garment of the palms and soles which [was] on him.
Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
24 And they took him and they threw him the pit towards and the pit [was] empty there not in it [was] water.
Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
25 And they sat down to eat bread and they lifted up eyes their and they saw and there! a caravan of Ishmaelites [was] coming from Gilead and camels their [were] carrying spice and balm and myrrh traveling to take [them] down Egypt towards.
Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
26 And he said Judah to brothers his what? [is the] profit if we will kill brother our and we will conceal blood his.
Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
27 Come and let us sell him to the Ishmaelites and hand our may not it be on him for [is] brother our flesh our he and they listened brothers his.
Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
28 And they passed by men Midianite[s] traders and they drew and they brought up Joseph from the pit and they sold Joseph to the Ishmaelites for twenty silver and they brought Joseph Egypt towards.
Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
29 And he returned Reuben to the pit and there! not Joseph [was] in the pit and he tore clothes his.
Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
30 And he returned to brothers his and he said the boy not [is] he and I where? [am] I going.
Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
31 And they took [the] long garment of Joseph and they slaughtered a male goat of goats and they dipped the long garment in the blood.
Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
32 And they sent [the] long garment of the palms and soles and they brought [it] to father their and they said this we have found investigate please ¿ [the] long garment of son your [is] it or? not.
Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
33 And he recognized it and he said [it is] [the] long garment of son my an animal wild it has eaten him certainly he has been torn to pieces Joseph.
Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
34 And he tore Jacob clothes his and he put sackcloth on loins his and he mourned on son his days many.
Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
35 And they arose all sons his and all daughters his to comfort him and he refused to be comforted and he said that I will go down to son my mourning Sheol towards and he wept for him father his. (Sheol h7585)
Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol h7585)
36 (And the Medanites *L(E)*) they sold him into Egypt to Potiphar an official of Pharaoh [the] commander of the bodyguards.
Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.

< Genesis 37 >