< Genesis 22 >

1 And it was after the things these and God he put to [the] test Abraham and he said to him O Abraham and he said here [am] I.
Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
2 And he said take please (son your *LA(bh)*) only [son] your whom you love Isaac and go for yourself to [the] land of Moriah and offer up him there to a burnt offering on one of the mountains which I will tell to you.
Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
3 And he rose early Abraham in the morning and he saddled donkey his and he took two of servants his with him and Isaac son his and he cut wood of burnt offering and he arose and he went to the place which he had said to him God.
Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
4 On the day third and he lifted up Abraham eyes his and he saw the place from a distance.
Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
5 And he said Abraham to servants his remain for yourselves here with the donkey and I and the lad we will go to there so we may bow down and we will return to you.
Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
6 And he took Abraham [the] wood of the burnt offering and he put [it] on Isaac son his and he took in hand his the fire and the knife and they went [the] two of them together.
Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
7 And he said Isaac to Abraham father his and he said O father my and he said here [am] I O son my and he said here! the fire and the wood and where? [is] the sheep for a burnt offering.
Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
8 And he said Abraham God he will see for himself the sheep for a burnt offering O son my and they went [the] two of them together.
Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
9 And they came to the place which he had said to him God and he built there Abraham the altar and he arranged the wood and he bound Isaac son his and he put him on the altar from above the wood.
Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
10 And he stretched out Abraham hand his and he took the knife to slaughter son his.
Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
11 And he called to him [the] angel of Yahweh from the heavens and he said O Abraham - Abraham and he said here [am] I.
Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
12 And he said may not you stretch out hand your against the lad and may not you do to him anything for - now I know that [are one] fearing God you and not you have withheld son your only [son] your from me.
Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
13 And he lifted up Abraham eyes his and he saw and there! a ram behind it was caught in the thicket by horns its and he went Abraham and he took the ram and he offered up it to a burnt offering in place of son his.
Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 And he called Abraham [the] name of the place that Yahweh - he will see that it is said this day on [the] mountain of Yahweh it will be seen.
Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
15 And he called [the] angel of Yahweh to Abraham a second [time] from the heavens.
Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
16 And he said by myself I swear [the] utterance of Yahweh that because that you have done the thing this and not you have withheld son your only [son] your.
akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
17 For surely I will bless you and certainly I will increase offspring your like [the] stars of the heavens and like the sand which [is] on [the] shore of the sea so may take possession of offspring your [the] gate of enemies its.
hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
18 And they will bless themselves by offspring your all [the] nations of the earth consequence that you have listened to voice my.
na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
19 And he returned Abraham to servants his and they arose and they went together to Beer Sheba and he dwelt Abraham in Beer Sheba.
Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
20 And it was after the things these and it was told to Abraham saying there! she has borne Milcah also she children to Nahor brother your.
Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
21 Uz firstborn his and Buz brother his and Kemuel [the] father of Aram.
Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
22 And Kesed and Hazo and Pildash and Jidlaph and Bethuel.
Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
23 And Bethuel he fathered Rebekah eight [sons] these she bore Milcah to Nahor [the] brother of Abraham.
Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
24 And concubine his and name her [was] Reumah and she bore also she Tebah and Gaham and Tahash and Maacah.
Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.

< Genesis 22 >