< Genesis 21 >
1 And Yahweh he visited Sarah just as he had said and he did Yahweh to Sarah just as he had spoken.
Wakati huu Bwana akamrehemu Sara kama alivyokuwa amesema, naye Bwana akamtendea Sara kile alichokuwa ameahidi.
2 And she conceived and she bore Sarah to Abraham a son of old age his to the appointed time which he had spoken with him God.
Sara akapata mimba, akamzalia Abrahamu mwana katika uzee wake, majira yale ya Mungu aliomwahidi.
3 And he called Abraham [the] name of son his who had been born to him whom she had borne to him Sarah Isaac.
Abrahamu akamwita Isaki yule mwana ambaye Sara alimzalia.
4 And he circumcised Abraham Isaac son his a son of eight days just as he had commanded him God.
Isaki alipokuwa na umri wa siku nane, Abrahamu akamtahiri, kama Mungu alivyomwamuru.
5 And Abraham [was] a son of one hundred year[s] when was born to him Isaac son his.
Abrahamu alikuwa na miaka 100 wakati Isaki mwanawe alipozaliwa.
6 And she said Sarah laughter he has made for me God everyone who hears he will laugh to me.
Sara akasema, “Mungu ameniletea kicheko, kila mmoja atakayesikia jambo hili atacheka pamoja nami.”
7 And she said who? has he said to Abraham she has suckled children Sarah for I have borne a son of old age his.
Akaongeza kusema, “Nani angemwambia Abrahamu kuwa Sara angenyonyesha watoto? Tena nimemzalia mwana katika uzee wake.”
8 And he grew up the child and he was weaned and he prepared Abraham a feast great on [the] day was weaned Isaac.
Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya. Siku hiyo Isaki alipoachishwa kunyonya, Abrahamu alifanya sherehe kubwa.
9 And she saw Sarah [the] son of Hagar the Egyptian whom she had borne to Abraham mocking.
Lakini Sara aliona kuwa mwana ambaye Hagari, Mmisri, aliyemzalia Abrahamu alikuwa anadhihaki,
10 And she said to Abraham drive out the slave woman this and son her for not he will inherit [the] son of the slave woman this with son my with Isaac.
Sara akamwambia Abrahamu, “Mwondoe mwanamke huyo mtumwa pamoja na mwanawe, kwa kuwa mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwanangu Isaki.”
11 And it was displeasing the matter exceedingly in [the] eyes of Abraham on [the] causes of son his.
Jambo hili lilimhuzunisha sana Abrahamu kwa sababu lilimhusu mwanawe.
12 And he said God to Abraham may not it be displeasing in view your on the lad and on slave woman your all that she says to you Sarah listen to voice her for in Isaac it will be named of you offspring.
Lakini Mungu akamwambia, “Usihuzunike hivyo kwa sababu ya kijana na mtumishi wako wa kike. Sikiliza lolote Sara analokuambia, kwa sababu uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.
13 And also [the] son of the slave woman into a nation I will make him for [is] offspring your he.
Nitamfanya huyu mwana wa mtumishi wako wa kike kuwa taifa pia, kwa sababu naye ni uzao wako.”
14 And he rose early Abraham - in the morning and he took food and a skin of water and he gave [them] to Hagar placing on shoulder her and the boy and he sent away her and she went and she wandered in [the] wilderness of Beer Sheba.
Kesho yake asubuhi na mapema, Abrahamu akachukua chakula na kiriba cha maji, akampa Hagari. Akaviweka mabegani mwa Hagari, akamwondoa pamoja na kijana. Hagari akashika njia, akatangatanga katika jangwa la Beer-Sheba.
15 And they were finished the water from the skin and she threw the boy under one of the bushes.
Maji yalipokwisha kwenye kiriba, akamwacha kijana chini ya mojawapo ya vichaka.
16 And she went and she sat for herself from before at a distance like [the] shooters of a bow for she said may not I look on [the] death of the boy and she sat from before and she lifted up voice her and she wept.
Kisha akajiendea zake akaketi karibu, umbali wa kutupa mshale, akawaza, “Siwezi kumwangalia kijana akifa.” Ikawa alipokuwa ameketi pale karibu, akaanza kulia kwa huzuni.
17 And he heard God [the] sound of the lad and he called [the] angel of God - to Hagar from the heavens and he said to her what? [is] to you O Hagar may not you be afraid for he has heard God [the] sound of the lad at where he [is] there.
Mungu akamsikia kijana akilia, malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni na kumwambia, “Kuna nini Hagari? Usiogope, Mungu amesikia kijana analia akiwa amelala pale.
18 Arise lift up the lad and take hold hand your on him for into a nation great I will make him.
Mwinue kijana na umshike mkono, kwa maana nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19 And he opened God eyes her and she saw a well of water and she went and she filled the skin water and she gave a drink to the lad.
Ndipo Mungu akamfumbua Hagari macho yake naye akaona kisima cha maji. Hivyo akaenda akajaza kiriba maji na kumpa kijana anywe.
20 And he was God with the lad and he grew up and he dwelt in the wilderness and he was a shooter a bowman.
Mungu akawa pamoja na huyu kijana alipokuwa akiendelea kukua. Aliishi jangwani na akawa mpiga upinde.
21 And he dwelt in [the] wilderness of Paran and she took for him mother his a wife from [the] land of Egypt.
Alipokuwa akiishi katika Jangwa la Parani, mama yake akampatia mke kutoka Misri.
22 And it was at the time that and he said Abimelech and Phicol [the] commander of army his to Abraham saying God [is] with you in all that you [are] doing.
Wakati huo Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakamwambia Abrahamu, “Mungu yu pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.
23 And therefore swear! to me by God here if you will deal falsely to me and to posterity my and to progeny my according to the loyalty which I have done with you you will do with me and with the land which you have sojourned in it.
Sasa niapie hapa mbele za Mungu kwamba hutanitenda hila mimi, watoto wangu wala wazao wangu. Nitendee mimi na nchi ambayo unaishi kama mgeni wema ule ule ambao nimekutendea.”
24 And he said Abraham I I will swear.
Abrahamu akasema, “Ninaapa hivyo.”
25 And he rebuked Abraham Abimelech on [the] causes of [the] well of water which they had seized [the] servants of Abimelech.
Ndipo Abrahamu akalalamika kwa Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamekinyangʼanya.
26 And he said Abimelech not I know who? has he done the thing this and also you not you told to me and also I not I heard except this day.
Lakini Abimeleki akasema, “Sijui ni nani ambaye amefanya hili. Hukuniambia, leo tu ndipo ninasikia habari zake.”
27 And he took Abraham sheep and cattle and he gave [them] to Abimelech and they made [the] two of them a covenant.
Hivyo Abrahamu akaleta kondoo na ngʼombe, akampa Abimeleki, nao watu hawa wawili wakafanya mapatano.
28 And he set Abraham seven ewe-lambs of the flock to alone them.
Abrahamu akatenga kondoo wa kike saba kutoka kwenye kundi,
29 And he said Abimelech to Abraham what? [are] they seven ewe-lambs these which you have set to alone them.
Abimeleki akamuuliza Abrahamu, “Ni nini maana ya hawa kondoo wa kike saba uliowatenga peke yao?”
30 And he said that seven ewe-lambs you will take from hand my in order that it may become for me a witness for I dug the well this.
Abrahamu akamjibu, “Upokee hawa kondoo wa kike saba kutoka mkononi mwangu kama ushahidi kuwa nilichimba kisima hiki.”
31 There-fore he called the place that Beer Sheba for there they swore an oath [the] two of them.
Hivyo mahali pale pakaitwa Beer-Sheba, kwa sababu watu wawili waliapiana hapo.
32 And they made a covenant at Beer Sheba and he arose Abimelech and Phicol [the] commander of army his and they returned to [the] land of [the] Philistines.
Baada ya mapatano kufanyika huko Beer-Sheba, Abimeleki na Fikoli mkuu wa majeshi yake wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33 And he planted a tamarisk tree in Beer Sheba and he called there on [the] name of Yahweh [the] God of perpetuity.
Abrahamu akapanda mti wa mkwaju huko Beer-Sheba, na hapo akaliitia jina la Bwana, Mungu wa milele.
34 And he sojourned Abraham in [the] land of [the] Philistines days many.
Naye Abrahamu akakaa katika nchi ya Wafilisti kwa muda mrefu.