< Genesis 10 >
1 And these [are] [the] accounts of [the] sons of Noah Shem Ham and Japheth and they were born to them sons after the flood.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 [the] sons of Japheth [were] Gomer and Magog and Madai and Javan and Tubal and Meshech and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 And [the] sons of Gomer [were] Ashkenaz and Riphath and Togarmah.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 And [the] sons of Javan [were] Elishah and Tarshish Kittim and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 From these they separated [the] coastlands of the nations in own lands their each to own language its to clans their in nations their.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 And [the] sons of Ham [were] Cush and Mizraim and Put and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 And [the] sons of Cush [were] Seba and Havilah and Sabtah and Raamah and Sabteca and [the] sons of Raamah [were] Sheba and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 And Cush he fathered Nimrod he he began to be a mighty [man] on the earth.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 He he was a mighty [man] of hunting before Yahweh there-fore it is said like Nimrod a mighty [man] of hunting before Yahweh.
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 And it was [the] beginning of kingdom his Babel and Erech and Akkad and Calneh in [the] land of Shinar.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 From the land that he went forth Assyria and he built Nineveh and Rehoboth-Ir and Calah.
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 And Resen between Nineveh and between Calah that [is] the city great.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 And Mizraim he fathered [the] Ludites and [the] Anamites and [the] Lehabites and [the] Naphtuhites.
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 And [the] Pathrusites and [the] Casluhites where they came out from there [the] Philistines and [the] Caphtorites.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 And Canaan he fathered Sidon firstborn his and Heth.
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 And the Jebusite[s] and the Amorite[s] and the Girgashite[s].
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 And the Hivite[s] and the Arkite[s] and the Sinite[s].
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 And the Arvadite[s] and the Zemarite[s] and the Hamathite[s] and after they were scattered [the] clans of the Canaanite[s].
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 And it was [the] border of the Canaanite[s] from Sidon going you Gerar towards to Gaza going you Sodom towards and Gomorrah and Admah and Zeboiim to Lasha.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 These [were] [the] sons of Ham to clans their to languages their in lands their in nations their.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 And to Shem was born also he [the] father of all [the] sons of Eber [the] brother of Japheth old.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 [the] sons of Shem [were] Elam and Asshur and Arphaxad and Lud and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 And [the] sons of Aram [were] Uz and Hul and Gether and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 And Arphaxad he fathered Shelah and Shelah he fathered Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 And to Eber was born two sons [the] name of the one [was] Peleg for in days his was divided the earth and [the] name of brother his [was] Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 And Joktan he fathered Almodad and Sheleph and Hazarmaveth and Jerah.
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 And Hadoram and Uzal and Diklah.
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 And Obal and Abimael and Sheba.
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 And Ophir and Havilah and Jobab all these [were] [the] sons of Joktan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 And it was dwelling place their from Mesha going you Sephar towards [the] hill country of the east.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 These [were] [the] sons of Shem to clans their to languages their in lands their to nations their.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 These [were] [the] clans of [the] sons of Noah to descendants their in nations their and from these they separated the nations on the earth after the flood.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.