< Ezekiel 32 >

1 And it was in two [plus] ten year in two [plus] ten month on [day] one of the month it came [the] word of Yahweh to me saying.
Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 O son of humankind take up a lamentation on Pharaoh [the] king of Egypt and you will say to him a young lion of nations you became like and you [were] like sea monster in the seas and you burst forth in rivers your and you made turbid waters with feet your and you fouled rivers their.
“Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
3 Thus he says [the] Lord Yahweh and I will spread over you net my by a company of peoples many and they will bring up you in net my.
Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
4 And I will abandon you on the land on [the] surface of the field I will throw you and I will cause to settle on you every bird of the heavens and I will satisfy from you [the] animal[s] of all the earth.
Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
5 And I will put flesh your on the mountains and I will fill the valleys height your.
Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
6 And I will make drink [the] land outflow your from blood your to the mountains and ravines they will be filled! from you.
Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
7 And I will cover when extinguishing you heavens and I will darken stars their [the] sun with cloud I will cover it and [the] moon not it will give light light its.
Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
8 All [the] luminaries of light in the heavens I will darken them over you and I will put darkness over land your [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
9 And I will disturb [the] heart of peoples many when bring I breaking your among the nations to lands which not you have known them.
Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
10 And I will make appalled on you peoples many and kings their they will shudder on you shuddering when brandish I sword my on faces their and they will tremble to moments everyone for life his on [the] day of downfall your.
Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
11 For thus he says [the] Lord Yahweh [the] sword of [the] king of Babylon it will come to you.
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
12 By [the] swords of warriors I will make fall multitude your ruthless [ones] of nations all of them and they will devastate [the] pride of Egypt and it will be destroyed all multitude its.
Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
13 And I will destroy all livestock its from at waters many and not it will make turbid them a foot of a human again and hooves of livestock not it will make turbid them.
Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
14 Then I will make settle waters their and rivers their like oil I will make go [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
15 When make I [the] land of Egypt a desolation and [is] made desolate [the] land from fullness its when strike down I all [the] inhabitants in it and they will know that I [am] Yahweh.
Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
16 [is] a lamentation It and people will chant it [the] daughters of the nations they will chant it over Egypt and over all multitude its they will chant it [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
17 And it was in two [plus] ten year on [day] fif-teen of the month it came [the] word of Yahweh to me saying.
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
18 O son of humankind wail on [the] multitude of Egypt and bring down it it and [the] daughters of nations mighty to [the] earth of [the] lowest parts with [those who] go down of [the] pit.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
19 More than whom? are you lovely go down! and be laid! with uncircumcised [men].
'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
20 In among [those] slain of a sword they will fall a sword it has been appointed they have drawn down it and all multitudes its.
Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
21 They will speak to him [the] leaders of [the] mighty [ones] from [the] midst of Sheol with helpers his they have come down they have lain down the uncircumcised [men] [those] slain of a sword. (Sheol h7585)
Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol h7585)
22 [is] there Assyria and all company its [are] around it graves its all of them [are] slain those [who] have fallen by the sword.
Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
23 Which they have been put graves its in [the] remotest parts of [the] pit and it was company its around grave its all of them [are] slain [those who] have fallen by the sword who they had put terror in [the] land of [the] living.
Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
24 [is] there Elam and all multitude its around grave its all of them [are] slain those [who] have fallen by the sword who they have gone down uncircumcised - into [the] earth of [the] lowest parts who they had put terror their in [the] land of [the] living and they have borne disgrace their with [those who] go down of [the] pit.
Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
25 In among [those] slain people have made a bed for it among all multitude its [are] around it graves its all of them [are] uncircumcised [those] slain of a sword for it was put terror their in [the] land of [the] living and they have borne disgrace their with [those who] go down of [the] pit in among [those] slain it was made.
Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
26 [is] there Meshech Tubal and all multitude its [are] around it graves its all of them [are] uncircumcised pierced of [the] sword for they had put terror their in [the] land of [the] living.
Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
27 And not they lie with warriors fallen from uncircumcised [men] who they went down Sheol with [the] weapons of war their and people put swords their under heads their and it was iniquities their on bones their for terror of warriors [was] in [the] land of [the] living. (Sheol h7585)
Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
28 And you in among uncircumcised [men] you will be broken and you may lie with [those] slain of a sword.
Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
29 [is] there Edom kings its and all princes its who they have been put in strength their with [those] slain of a sword they with uncircumcised [men] they will lie and with [those who] go down of [the] pit.
Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
30 [are] there Princes of [the] north all of them and all [the] Sidonian[s] who they have gone down with [those] slain in terror their (from strength their *LA(bh)*) being ashamed and they lay uncircumcised with [those] slain of a sword and they have borne disgrace their with [those who] go down of [the] pit.
Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
31 Them he will see Pharaoh and he will be comforted on all (multitude his *Q(K)*) [those] slain of a sword Pharaoh and all army his [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
32 That I had put (terror my *Q(K)*) in [the] land of [the] living and he will be laid in among uncircumcised [men] with [those] slain of a sword Pharaoh and all (multitude his *Q(K)*) [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.

< Ezekiel 32 >