< Ezekiel 19 >
1 And you take up a lamentation because of [the] princes of Israel.
“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
2 And you will say what? [was] mother your a lioness between lions she lay down in among young lions she reared cubs her.
na useme: “‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
3 And she brought up one of cubs her a young lion it was and it learned to tear prey human[s] it devoured.
Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
4 And they heard concerning it nations in pit their it was caught and they brought it with hooks to [the] land of Egypt.
Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana mpaka nchi ya Misri.
5 And she saw that she waited it was lost hope her and she took one of cubs her a young lion she made it.
“‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
6 And it went about in among lions a young lion it was and it learned to tear prey human[s] it devoured.
Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
7 And it knew widows its and cities their it laid waste and it was desolate [the] land and what fills it from [the] sound of roaring its.
Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
8 And they set on it nations all around from provinces and they spread out over it net their in pit their it was caught.
Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
9 And they put it in cage with hooks and they brought it to [the] king of Babylon they brought it in strongholds so that not it will be heard voice its again to [the] mountains of Israel.
Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli. Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
10 Mother your like vine in blood your at water planted fruitful and full of branches it was from waters many.
“‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
11 And they belonged to it branches of strength to scepters of rulers and it was lofty stature its above between branches and it was seen by height its by [the] abundance of branches its.
Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
12 And it was plucked up in rage to the ground it was thrown down and [the] wind of the east it dried up fruit its they were torn off and they became dry [the] branch of strength its a fire it consumed it.
Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
13 And now [it is] planted in the wilderness in a land dry and thirst.
Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
14 And it went out fire from [the] branch of shoots its fruit its it consumed and not it was in it a branch of strength a scepter to rule [is] a lamentation it and it has become a lamentation.
Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”