< Ezekiel 18 >
1 And it came [the] word of Yahweh to me saying.
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 What? [is] to you you [are] speaking a proverb the proverb this on [the] land of Israel saying parents they eat sour grape[s] and [the] teeth of the children (they are blunt. *LA(bh)*)
“Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli: “‘Baba wamekula zabibu zenye chachu, nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?
3 [by] [the] life Of me [the] utterance of [the] Lord Yahweh if it will belong to you again to speak a proverb the proverb this in Israel.
“Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli.
4 Here! all lives [belong] to me they as [the] life of the parent and as [the] life of the child [belong] to me they the soul which sins it it will die.
Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.
5 And anyone for he will be righteous and he will do justice and righteousness.
“Mtu aweza kuwa ni mwenye haki atendaye yaliyo haki na sawa.
6 To the mountains not he has eaten and eyes his not he has lifted up to [the] idols of [the] house of Israel and [the] wife of neighbor his not he has defiled and to a woman menstruation not he drew near.
Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima wala hakuziinulia macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake, wala hakukutana kimwili na mwanamke wakati wa siku zake za hedhi.
7 And anyone not he oppressed pledge his a debt he returned robbery not he robbed food his to [the] hungry he gave and [the] naked he covered clothing.
Hamwonei mtu yeyote, bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
8 For interest not he lent and interest not he took from injustice he turned away hand his justice of faithfulness he did between a person and a person.
Hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huuzuia mkono wake usifanye mabaya, naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.
9 In statutes my he walked and judgments my he has kept by doing faithfulness [is] righteous he certainly he will live [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
Huzifuata amri zangu na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu. Huyo mtu ni mwenye haki; hakika ataishi, asema Bwana Mwenyezi.
10 And he will father a son violent [who] sheds blood and he will do alas! any one of these [things].
“Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya
11 And he all these [things] not he did for also to the mountains he has eaten and [the] wife of neighbor his he has defiled.
(ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya): “Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima. Humtia unajisi mke wa jirani yake.
12 [the] poor And [the] needy he has oppressed robberies he has robbed a pledge not he returned and to the idols he has lifted up eyes his abomination he has done.
Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.
13 For interest he has lent and interest he has taken and will he live? not he will live all the abominations these he has done certainly he will be put to death blood his on him it will be.
Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada. Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
14 And there! he has fathered a child and he has seen all [the] sins of father his which he did and he saw and not he did like them.
“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:
15 On the mountains not he has eaten and eyes his not he has lifted up to [the] idols of [the] house of Israel [the] wife of neighbor his not he has defiled.
“Hakula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima, wala hainulii macho sanamu za nyumba ya Israeli. Hakumtia unajisi mke wa jirani yake.
16 And anyone not he has oppressed a pledge not he has taken as pledge and robbery not he has robbed food his to [the] hungry he has given and [the] naked he has covered clothing.
Hakumwonea mtu yeyote wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo. Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake na huwapa nguo walio uchi.
17 From [the] poor he has turned away hand his interest and interest not he has taken judgments my he has done in statutes my he has walked he not he will die for [the] iniquity of father his certainly he will live.
Huuzuia mkono wake usitende dhambi, hakopeshi kwa riba wala hajipatii faida ya ziada. Huzishika amri zangu na kuzifuata sheria zangu. Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi.
18 Father his for he has extorted extortion he has robbed robbery of a brother and [that] which not [was] good he has done in among people his and there! he will die for iniquity his.
Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.
19 And you say why? not has he borne the child in [the] iniquity of the parent and the child justice and righteousness he has done all statutes my he has kept and he has done them certainly he will live.
“Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi.
20 The soul which sins it it will die a child not he will bear - in [the] iniquity of the parent and a parent not he will bear in [the] iniquity of the child [the] righteousness of the righteous [person] on him it will be and [the] wickedness of (the wicked [person] *Q(K)*) on him it will be.
Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.
21 And the wicked [person] if he will turn away from all (sins his *Q(K)*) which he has done and he will keep all (statutes my *LAB(h)*) and he will do justice and righteousness certainly he will live not he will die.
“Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa.
22 All transgressions his which he has done not they will be remembered to him for righteousness his which he has done he will live.
Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi.
23 ¿ Really do I take pleasure in [the] death of [the] wicked [the] utterance of [the] Lord Yahweh ¿ not when turning back he from ways his and he will live.
Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?
24 And when turns away [the] righteous from righteousness his and he will do injustice according to all the abominations which he did the wicked [person] he will do and will he live? all (righteousness his *Q(K)*) which he did not they will be remembered for unfaithfulness his which he has acted unfaithfully and for sin his which he has sinned for them he will die.
“Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.
25 And you say not it is correct [the] way of [the] Lord listen please O house of Israel ¿ way my not is it correct ¿ not ways your not are they correct.
“Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?
26 When turns away [the] righteous from righteousness his and he will do injustice and he will die on them for injustice his which he has done he will die.
Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa.
27 And when turns away [the] wicked from wickedness his which he has done and he did justice and righteousness he life his he will preserve alive.
Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake.
28 And he saw (and he turned away *Q(k)*) from all transgressions his which he had done certainly he will live not he will die.
Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa.
29 And they say [the] house of Israel not it is correct [the] way of [the] Lord ¿ ways my not are they correct O house of Israel ¿ not ways your not is it correct.
Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”
30 Therefore everyone according to ways his I will judge you O house of Israel [the] utterance of [the] Lord Yahweh turn back and turn away from all transgressions your and not it will become for you a stumbling block iniquity.
“Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu.
31 Throw away from with you all transgressions your which you have transgressed by them and make for yourselves a heart new and a spirit new and why? will you die O house of Israel.
Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli?
32 For not I take pleasure in [the] death of the [one who] dies [the] utterance of [the] Lord Yahweh and turn away and live.
Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!