< Exodus 6 >

1 And he said Yahweh to Moses now you will see [that] which I will do to Pharaoh for by a hand strong he will let go them and by a hand strong he will drive out them from land his.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Sasa utaona kitu nitakachomfanyia Farao: Kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawaachia watu waende; kwa sababu ya mkono wangu wenye nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”
2 And he spoke God to Moses and he said to him I [am] Yahweh.
Pia Mungu akamwambia Mose, “Mimi ndimi Bwana.
3 And I appeared to Abraham to Isaac and to Jacob God Almighty and name my Yahweh not I made myself known to them.
Nilimtokea Abrahamu, Isaki na Yakobo kama Mungu Mwenyezi, ingawa sikuwajulisha Jina langu, Yehova, Mimi mwenyewe sikujitambulisha kwao.
4 And also I established covenant my with them to give to them [the] land of Canaan [the] land of sojournings their which they sojourned in it.
Pia niliweka Agano langu nao kuwapa nchi ya Kanaani, ambako waliishi kama wageni.
5 And also - I I have heard [the] groaning of [the] people of Israel whom Egypt [are] compelling to labor them and I have remembered covenant my.
Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha huzuni cha Waisraeli ambao Wamisri wamewatia utumwani, nami nimelikumbuka Agano langu.
6 Therefore say to [the] people of Israel I [am] Yahweh and I will bring out you from under [the] forced labor of Egypt and I will deliver you from labor their and I will redeem you by an arm outstretched and with acts of judgment great.
“Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ndimi Bwana, nami nitawatoa mtoke katika kongwa la Wamisri. Nitawaweka huru mtoke kuwa watumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa pamoja na matendo makuu ya hukumu.
7 And I will take you for myself to a people and I will become for you God and you will know that I [am] Yahweh God your who brought out you from under [the] forced labor of Egypt.
Nitawatwaa mwe watu wangu mwenyewe, nami nitakuwa Mungu wenu. Ndipo mtajua kuwa mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa chini ya kongwa la Wamisri.
8 And I will bring you into the land which I lifted up hand my to give it to Abraham to Isaac and to Jacob and I will give it to you a possession I [am] Yahweh.
Nami nitawaleta mpaka nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kumpa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Nitawapa iwe milki yenu. Mimi ndimi Bwana.’”
9 And he spoke Moses thus to [the] people of Israel and not they listened to Moses from shortness of spirit and from labor hard.
Mose akawaarifu Waisraeli jambo hili, lakini hawakumsikiliza kwa sababu ya maumivu makuu ya moyoni na utumwa wa kikatili.
10 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Ndipo Bwana akamwambia Mose,
11 Go speak to Pharaoh [the] king of Egypt so he may let go [the] people of Israel from land his.
“Nenda, mwambie Farao mfalme wa Misri awaachie Waisraeli waondoke nchini mwake.”
12 And he spoke Moses before Yahweh saying here! [the] people of Israel not they have listened to me and how? will he listen to me Pharaoh and I [am] uncircumcised of lips.
Lakini Mose akamwambia Bwana, “Ikiwa Waisraeli hawatanisikiliza, kwa nini yeye Farao anisikilize mimi, ambaye huzungumza kwa kigugumizi?”
13 And he spoke Yahweh to Moses and to Aaron and he commanded them to [the] people of Israel and to Pharaoh [the] king of Egypt to bring out [the] people of Israel from [the] land of Egypt.
Ndipo Bwana akanena na Mose na Aroni kuhusu Waisraeli na Farao mfalme wa Misri, naye akawaamuru wawatoe Waisraeli kutoka Misri.
14 These [were] [the] heads of [the] household of ancestors their [the] sons of Reuben [the] firstborn of Israel [were] Hanoch and Pallu Hezron and Carmi these [were] [the] clans of Reuben.
Hawa walikuwa wakuu wa jamaa zao: Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli walikuwa Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hawa walikuwa ndio koo za Reubeni.
15 And [the] sons of Simeon [were] Jemuel and Jamin and Ohad and Jakin and Zohar and Shaul [the] son of Canaanite [woman] these [were] [the] clans of Simeon.
Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. Hawa walikuwa ndio koo za Simeoni.
16 And these [were] [the] names of [the] sons of Levi to descendants their Gershon and Kohath and Merari and [the] years of [the] life of Levi [were] seven and thirty and one hundred year[s].
Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi kufuatana na orodha zao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137.
17 [the] sons of Gershon [were] Libni and Shimei to clans their.
Wana wa Gershoni kwa koo, walikuwa Libni na Shimei.
18 And [the] sons of Kohath [were] Amram and Izhar and Hebron and Uzziel and [the] years of [the] life of Kohath [were] three and thirty and one hundred year[s].
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133.
19 And [the] sons of Merari [were] Mahli and Mushi these [were] [the] clans of the Levite[s] to descendants their.
Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Lawi kufuatana na orodha zao.
20 And he took Amram Jochebed father's sister his for himself to a wife and she bore to him Aaron and Moses and [the] years of [the] life of Amram [were] seven and thirty and one hundred year[s].
Amramu akamwoa Yokebedi, shangazi yake, ambaye alimzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
21 And [the] sons of Izhar [were] Korah and Nepheg and Zikri.
Wana wa Ishari walikuwa Kora, Nefegi na Zikri.
22 And [the] sons of Uzziel [were] Mishael and Elzaphan and Sithri.
Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elisafani na Sithri.
23 And he took Aaron Elisheba [the] daughter of Amminadab [the] sister of Nahshon for himself to a wife and she bore to him Nadab and Abihu Eleazar and Ithamar.
Aroni akamwoa Elisheba binti wa Aminadabu ndugu yake Nashoni, naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
24 And [the] sons of Korah [were] Assir and Elkanah and Abiasaph these [were] [the] clans of the Korahite[s].
Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasafu. Hawa walikuwa ndio koo za Kora.
25 And Eleazar [the] son of Aaron he took for himself one of [the] daughters of Putiel for himself to a wife and she bore to him Phinehas these [were] [the] heads of [the] ancestors of the Levites to clans their.
Eleazari mwana wa Aroni akamwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa walikuwa ndio wakuu wa jamaa za Walawi, ukoo kwa ukoo.
26 That Aaron and Moses whom he said Yahweh to them bring out [the] people of Israel from [the] land of Egypt on hosts their.
Hawa walikuwa Aroni na Mose wale wale ambao Bwana aliwaambia, “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.”
27 They [were] the [ones who] were speaking to Pharaoh [the] king of Egypt to bring out [the] people of Israel from Egypt that Moses and Aaron.
Ndio hao hao waliozungumza na Farao mfalme wa Misri kuhusu kuwatoa Waisraeli Misri. Ilikuwa ni huyo Mose na huyo Aroni.
28 And it was on [the] day [when] he spoke Yahweh to Moses in [the] land of Egypt.
Bwana aliponena na Mose huko Misri,
29 And he spoke Yahweh to Moses saying I [am] Yahweh speak to Pharaoh [the] king of Egypt all that I [am] speaking to you.
akamwambia, “Mimi ndimi Bwana. Mwambie Farao mfalme wa Misri kila kitu nikuambiacho.”
30 And he said Moses before Yahweh here! I [am] uncircumcised of lips and how? will he listen to me Pharaoh.
Lakini Mose akamwambia Bwana, “Kwa kuwa mimi huzungumza kwa kigugumizi, Farao atanisikiliza mimi?”

< Exodus 6 >