< Exodus 36 >
1 And he will do Bezalel and Oholiab and every - person skillful of heart whom he has put Yahweh skill and understanding in them to know to do all [the] work of [the] service of the holy place to all that he has commanded Yahweh.
Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
2 And he called Moses to Bezalel and to Oholiab and to every person skillful of heart whom he had put Yahweh skill in heart his every [one] whom it lifted him heart his to draw near to the work to do it.
Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
3 And they received from to before Moses all the contribution which they had brought [the] people of Israel for [the] work of [the] service of the holy place to do it and they they brought to him still a freewill offering in the morning in the morning.
Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
4 And they came all the skillful [people] who were doing all [the] work of the holy place person person from work his which they [were] doing.
Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
5 And they said to Moses saying [are] multiplying the people to bring more than sufficiency of the service for the work which he has commanded Yahweh to do it.
wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
6 And he commanded Moses and they caused to pass a proclamation in the camp saying a man and a woman may not they make again work for [the] contribution of the holy place and it was restrained the people from bringing.
Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
7 And the work it was sufficiency their for all the work to do it and it was more than enough.
kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
8 And they made every [person] skillful of heart among [those who] did the work the tabernacle ten curtains fine linen twisted and violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet cherubim [the] work of a skillful worker he made them.
Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
9 [the] length of The curtain one [was] eight and twenty by the cubit and [the] breadth [was] four by the cubit the curtain one size one [belonged] to all the curtains.
Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
10 And he joined five of the curtains one to one and five curtains he joined one to one.
Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
11 And he made loops of violet stuff on [the] edge of the curtain one from an end in the joined set thus he did on [the] edge of the curtain outermost in the joined set second.
Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
12 Fifty loops he made on the curtain one and fifty loops he made on [the] edge of the curtain which [was] in the joined set second [were] opposite the loops one to one.
Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
13 And he made fifty hooks of gold and he joined the curtains one to one with the hooks and it was the tabernacle one.
Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
14 And he made curtains of goat hair into a tent over the tabernacle one [plus] ten curtains he made them.
Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
15 [the] length of The curtain one [was] thirty by the cubit and [was] four cubits [the] breadth of the curtain one size one [belonged] to one [plus] ten curtains.
Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
16 And he joined five of the curtains alone and six of the curtains alone.
Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
17 And he made loops fifty on [the] edge of the curtain outermost in the joined set and fifty loops he made on [the] edge of the curtain the joined set second.
Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
18 And he made hooks of bronze fifty to join together the tent to be one.
Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
19 And he made a covering for the tent skins of rams dyed red and a covering of skins of dolphins from to above.
Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
20 And he made the frames for the tabernacle wood of acacia standing upright.
Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
21 [was] ten (Cubits *L(abh)*) [the] length of the frame and [was] a cubit and [the] half of cubit [the] breadth of the frame one.
Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
22 Two hands [belonged] to the frame the one joined one to one thus he did for all [the] frames of the tabernacle.
zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
23 And he made the frames for the tabernacle twenty frames for [the] side of [the] south south-ward.
Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
24 And forty bases of silver he made under twenty the frames two bases [were] under the frame one for [the] two hands its and two bases [were] under the frame one for [the] two hands its.
na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
25 And for [the] side of the tabernacle second to [the] side of [the] north he made twenty frames.
Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
26 And forty bases their silver two bases [were] under the frame one and two bases [were] under the frame one.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
27 And for [the] innermost parts of the tabernacle west-ward he made six frames.
Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
28 And two frames he made for [the] corners of the tabernacle in the innermost parts.
na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
29 And they were twins from to downwards and together they were complete to top its into the ring one thus he did for [the] two of them for [the] two the corners.
Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
30 And they were eight frames and bases their [were] silver six-teen bases two bases two bases [were] under the frame one.
Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
31 And he made bars of wood of acacia five [bars] for [the] frames of [the] side of the tabernacle one.
Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
32 And five bars for [the] frames of [the] side of the tabernacle second and five bars for [the] frames of the tabernacle for the innermost parts west-ward.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
33 And he made the bar middle to pass through in [the] middle of the frames from the end to the end.
Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
34 And the frames he overlaid gold and rings their he made gold holders for the bars and he overlaid the bars gold.
Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
35 And he made the curtain violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted [the] work of a skillful worker he made it cherubim.
Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
36 And he made for it four pillars of acacia and he overlaid them gold hooks their [were] gold and he cast for them four bases of silver.
Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
37 And he made a screen for [the] entrance of the tent violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted [the] work of a worker in colors.
Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
38 And pillars its five and hooks their and he overlaid tops their and bands their gold and bases their five [were] bronze.
Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.