< Exodus 32 >

1 And it saw the people that he delayed Moses to come down from the mountain and it assembled the people to Aaron and they said to him arise - make for us gods which they will go before us for this - Moses the man who he brought up us from [the] land of Egypt not we know what? has it happened to him.
Watu walipoona kuwa Mose amekawia sana kushuka kutoka mlimani, walimkusanyikia Aroni na kumwambia, “Njoo, tutengenezee miungu itakayotutangulia. Kwa maana huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatujui jambo lililompata.”
2 And he said to them Aaron tear off [the] rings of gold which [are] on [the] ears of wives your sons your and daughters your and bring [them] to me.
Aroni akawajibu, “Vueni vipuli vya dhahabu ambavyo wake zenu, wana wenu na binti zenu wamevaa, mkaniletee.”
3 And they tore off from themselves all the people [the] rings of gold which [were] on ears their and they brought [them] to Aaron.
Kwa hiyo watu wote wakavua vipuli vyao, wakavileta kwa Aroni.
4 And he took [them] from hand their and he fashioned it with tool and he made it a calf of molten metal and they said these [are] gods your O Israel who they brought up you from [the] land of Egypt.
Akavichukua vile vitu walivyomkabidhi, akavifanyiza kwa kusubu sanamu yenye umbo la ndama, akaichonga kwa kutumia chombo. Kisha wakasema, “Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
5 And he saw Aaron and he built an altar before it and he called Aaron and he said a festival of Yahweh [will be] tomorrow.
Aroni alipoona hili, akajenga madhabahu mbele ya yule ndama na kutangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa Bwana.”
6 And they rose early from [the] next day and they offered up burnt offerings and they brought near peace offerings and it sat down the people to eat and to drink and they arose to play.
Kwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha katika sherehe.
7 And he spoke Yahweh to Moses go go down for it has behaved corruptly people your which you brought up from [the] land of Egypt.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Shuka, kwa sababu watu wako, uliowatoa Misri, wamepotoka.
8 They have turned aside quickly from the way which I commanded them they have made for themselves a calf of molten metal and they have bowed down to it and they have sacrificed to it and they have said these [are] gods your O Israel who they brought up you from [the] land of Egypt.
Wamekuwa wepesi kugeuka na kuacha niliyowaamuru, na wamejitengenezea sanamu ya kuyeyusha yenye umbo la ndama. Wameisujudia na kuitolea dhabihu, nao wamesema, ‘Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli iliyokupandisha kutoka Misri.’”
9 And he said Yahweh to Moses I have seen the people this and there! [is] a people stiff of neck it.
Bwana akamwambia Mose, “Nimeona watu hawa, nao ni watu wenye shingo ngumu.
10 And therefore leave alone! me so may it burn anger my on them so I may make an end of them and I may make you into a nation great.
Sasa niache ili hasira yangu ipate kuwaka dhidi yao, nami nipate kuwaangamiza. Kisha nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa.”
11 And he entreated Moses [the] face of Yahweh God his and he said why? O Yahweh does it burn anger your on people your which you brought out from [the] land of Egypt with power great and by a hand strong.
Lakini Mose akamsihi Bwana Mungu wake, akasema, “Ee Bwana, kwa nini hasira yako iwake dhidi ya watu wako, wale uliowatoa Misri kwa uweza mkuu na mkono wenye nguvu?
12 Why? will they say Egypt saying with evil he brought out them to kill them in the mountains and to make an end of them from on [the] surface of the ground turn from [the] burning of anger your and relent on the harm to people your.
Kwa nini Wamisri waseme, ‘Ni kwa nia mbaya aliwatoa Misri, ili awaue milimani na kuwafuta usoni mwa dunia’? Achilia mbali hasira yako kali, waonee huruma na usilete maafa juu ya watu wako.
13 Remember Abraham Isaac and Israel servants your whom you swore to them by yourself and you said to them I will increase offspring your like [the] stars of the heavens and all the land this which I have promised I will give to offspring your and they will possess [it] for ever.
Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaki na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe: ‘Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa wazao wako nchi hii yote ambayo niliwaahidia, nayo itakuwa urithi wao milele.’”
14 And he relented Yahweh on the harm which he had spoken to do to people his.
Kisha Bwana akawaonea huruma, wala hakuleta juu ya watu wake maafa aliyokuwa amekusudia.
15 And he turned and he went down Moses from the mountain and [the] two [the] tablets of the testimony [were] in hand his tablets written from [the] two sides their from this and from this they [were] written.
Mose akageuka, akashuka kutoka mlimani akiwa na vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake. Vilikuwa vimeandikwa pande zote mbili, mbele na nyuma.
16 And the tablets [were] [the] work of God they and the writing [was] [the] writing of God it engraved on the tablets.
Vibao hivyo vilikuwa kazi ya Mungu; maandishi yalikuwa mwandiko wa Mungu, yaliyochorwa kama muhuri juu ya vibao.
17 And he heard Joshua [the] sound of the people (in shouting its *Q(K)*) and he said to Moses a sound of battle [is] in the camp.
Yoshua aliposikia sauti za watu wakipiga kelele, akamwambia Mose, “Kuna sauti ya vita kambini.”
18 And he said there not [is] a sound of singing of strength and there not [is] a sound of singing of weakness a sound of singing I [am] hearing.
Mose akajibu: “Si sauti ya ushindi, wala si sauti ya kushindwa; ni sauti ya kuimba ninayosikia.”
19 And it was just when he drew near to the camp and he saw the calf and dancing and it burned [the] anger of Moses and he threw down (from hands his *Q(K)*) the tablets and he broke in pieces them under the mountain.
Mose alipoikaribia kambi na kuona yule ndama na ile michezo, hasira yake ikawaka, akatupa vile vibao vilivyokuwa mikononi mwake, akavipasua vipande vipande pale chini ya mlima.
20 And he took the calf which they had made and he burned [it] with fire and he ground [it] until that it was fine and he scattered [it] on [the] surface of the water and he made drink [it] [the] people of Israel.
Kisha akamchukua yule ndama waliokuwa wamemtengeneza na kumchoma kwenye moto, kisha akamsaga kuwa unga, akanyunyiza kwenye maji na kuwafanya Waisraeli wanywe.
21 And he said Moses to Aaron what? did it do to you the people this that you have brought on it a sin great.
Mose akamwambia Aroni, “Watu hawa walikufanyia nini, hata ukawaongoza kufanya dhambi kubwa hivyo?”
22 And he said Aaron may not it burn [the] anger of lord my you you know the people that [is] on evil it.
Aroni akamwambia, “Usikasirike bwana wangu. Unajua jinsi watu hawa walivyo tayari kwa maovu.
23 And they said to me make for us gods which they will go before us for this - Moses the man who he brought up us from [the] land of Egypt not we know what? has it happened to him.
Wao waliniambia, ‘Tufanyie miungu itakayotuongoza. Kwa kuwa huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatufahamu yaliyompata.’
24 And I said to them [belongs] to whom? gold tear [it] off from yourselves and they gave [it] to me and I threw it in the fire and it came out the calf this.
Kwa hiyo nikawaambia, ‘Yeyote aliye na kito chochote cha dhahabu avue.’ Kisha wakanipa hiyo dhahabu, nami nikaitupa motoni, akatokea huyu ndama!”
25 And he saw Moses the people for [was] running wild it for had let [it] run wild he Aaron for derision among [those who] rise against them.
Mose akaona kuwa watu wameasi, kwa kuwa Aroni alikuwa amewaacha waasi, na hivyo kuwa kichekesho kwa adui zao.
26 And he stood Moses at [the] gate of the camp and he said who? [belongs] to Yahweh to me and they gathered themselves to him all [the] descendants of Levi.
Kwa hiyo Mose akasimama kwenye ingilio la kambi, akasema, “Yeyote aliye upande wa Bwana, aje upande wangu.” Walawi wote wakamjia.
27 And he said to them thus he says Yahweh [the] God of Israel put everyone sword his on thigh his pass and return from gate to gate in the camp and kill everyone brother his and everyone friend his and everyone neighbor his.
Ndipo alipowaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Kila mmoja wenu ajifunge upanga wake kiunoni aende huku na huko kambi yote mwisho hadi mwisho mwingine, kila mmoja amuue ndugu yake, na rafiki yake na jirani yake.’”
28 And they did [the] descendants of Levi according to [the] word of Moses and it fell of the people on the day that about three thousand person[s].
Walawi wakafanya kama Mose alivyoamuru, siku ile wakafa watu wapatao 3,000.
29 And he said Moses fill hand your this day to Yahweh for everyone [was] on son his and on brother his and to put on yourselves this day a blessing.
Kisha Mose akasema, “Leo mmewekwa wakfu kwa Bwana, kwa kuwa mlikuwa kinyume na wana wenu wenyewe na ndugu zenu, naye Mungu amewabariki leo.”
30 And it was from [the] next day and he said Moses to the people you you have sinned a sin great and now I will go up to Yahweh perhaps I will atone for sin your.
Siku iliyofuata Mose akawaambia watu, “Mmefanya dhambi kubwa. Lakini sasa nitapanda juu kwa Bwana, labda nitaweza kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
31 And he returned Moses to Yahweh and he said I beg you it has sinned the people this a sin great and they have made for themselves gods of gold.
Hivyo Mose akarudi kwa Bwana na kumwambia, “Lo! Hawa watu wamefanya dhambi kubwa namna gani! Wamejitengenezea miungu ya dhahabu.
32 And therefore if you will forgive sin their and if not wipe out me please from book your which you have written.
Lakini sasa nakusihi, wasamehe dhambi yao; lakini kama sivyo, basi nifute kutoka kwenye kitabu ulichoandika.”
33 And he said Yahweh to Moses who? [is [the] one] who he has sinned to me I will wipe out him from book my.
Bwana akamjibu Mose, “Yeyote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta kutoka kwenye kitabu changu.
34 And now go - lead the people to where I have spoken to you there! angel my he will go before you and on [the] day visit I and I will visit on them sin their.
Sasa nenda, uongoze hao watu mpaka mahali nilipokuambia, naye malaika wangu atakutangulia. Pamoja na hayo, wakati utakapofika wa mimi kuwaadhibu, nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi yao.”
35 And he struck Yahweh the people on that they had made the calf which he had made Aaron.
Ndipo Bwana akawapiga watu kwa ugonjwa wa tauni kwa sababu ya yale waliyoyafanya kwa ndama yule ambaye alitengenezwa na Aroni.

< Exodus 32 >