< Exodus 3 >

1 And Moses he was pasturing [the] flock of Jethro father-in-law his [the] priest of Midian and he drove the flock behind the wilderness and he came to [the] mountain of God Horeb towards.
Basi Mose alikuwa anachunga mifugo ya Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani. Mose akapeleka mifugo mbali nyuma ya jangwa, naye akafika Horebu, mlima wa Mungu.
2 And he appeared [the] angel of Yahweh to him in a flame of fire from [the] middle of the bush and he saw and there! the bush [was] burning with fire and the bush not it [was] consumed.
Huko malaika wa Bwana akamtokea Mose katika mwali wa moto kutoka kichakani. Mose akaona kwamba ingawa kile kichaka kilikuwa kinawaka moto, kilikuwa hakiteketei.
3 And he said Moses I will turn aside please so I may see the sight great this why? not is it burning the bush.
Ndipo Mose akawaza, “Nitageuka sasa nione kitu hiki cha ajabu, nami nione ni kwa nini kichaka hiki hakiteketei.”
4 And he saw Yahweh that he had turned aside to look and he called to him God from [the] middle of the bush and he said O Moses Moses and he said here [am] I.
Bwana alipoona kuwa amegeuka ili aone, Mungu akamwita kutoka ndani ya kile kichaka, “Mose! Mose!” Naye Mose akajibu, “Mimi hapa.”
5 And he said may not you draw near here take off sandals your from on feet your for the place which you [are] standing on it [is] ground of holiness it.
Mungu akamwambia, “Usikaribie zaidi. Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni patakatifu.”
6 And he said I [am] [the] God of father your [the] God of Abraham [the] God of Isaac and [the] God of Jacob and he hid Moses face his for he was afraid from looking to God.
Kisha akamwambia, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.” Mose aliposikia hayo, akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumtazama Mungu.
7 And he said Yahweh certainly I have seen [the] affliction of people my which [is] in Egypt and cry of distress their I have heard because of taskmasters its for I know pains its.
Bwana akamwambia, “Hakika nimeona mateso ya watu wangu katika Misri. Nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao, nami naguswa na mateso yao.
8 And I have come down to deliver it - from [the] hand of Egypt and to bring up it from the land that into a land good and spacious into a land flowing of milk and honey to [the] place of the Canaanite[s] and the Hittite[s] and the Amorite[s] and the Perizzite[s] and the Hivite[s] and the Jebusite[s].
Basi nimeshuka niwaokoe kutoka mkono wa Wamisri, niwatoe na kuwapandisha kutoka nchi hiyo, niwapeleke katika nchi nzuri na kubwa, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9 And now there! [the] cry of distress of [the] people of Israel it has come to me and also I have seen the oppression which Egypt [are] oppressing them.
Sasa kilio cha Waisraeli kimenifikia, nami nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.
10 And therefore go! and I will send you to Pharaoh and bring out people my [the] people of Israel from Egypt.
Basi, sasa nenda. Ninakutuma kwa Farao ili kuwatoa watu wangu Waisraeli kutoka Misri.”
11 And he said Moses to God who? [am] I that I will go to Pharaoh and that I will bring out [the] people of Israel from Egypt.
Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao kuwatoa Waisraeli nchini Misri?”
12 And he said that I will be with you and this for you [will be] the sign that I I sent you when bringing out you the people from Egypt you will serve! God on the mountain this.
Naye Mungu akasema, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako kwamba ni Mimi nimekutuma: Hapo utakapokuwa umewatoa watu Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.”
13 And he said Moses to God here! I [am] about to go to [the] people of Israel and I will say to them [the] God of ancestors your he has sent me to you and they will say to me what? [is] name his what? will I say to them.
Mose akamwambia Mungu, “Ikiwa nitawaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani?’ Nitawaambia nini?”
14 And he said God to Moses I am [that] which I am and he said thus you will say to [the] people of Israel I am he has sent me to you.
Mungu akamwambia Mose, “Mimi niko ambaye niko. Hivyo ndivyo utakavyowaambia Waisraeli: ‘Mimi niko amenituma kwenu.’”
15 And he said again God to Moses thus you will say to [the] people of Israel Yahweh [the] God of ancestors your [the] God of Abraham [the] God of Isaac and [the] God of Jacob he has sent me to you this [is] name my for ever and this [is] memorial my to a generation generation.
Vilevile Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo amenituma kwenu.’ Hili ndilo Jina langu milele, Jina ambalo mtanikumbuka kwalo kutoka kizazi hadi kizazi.
16 Go and you will gather [the] elders of Israel and you will say to them Yahweh [the] God of ancestors your he appeared to me [the] God of Abraham Isaac and Jacob saying certainly I have observed you and the [thing] done to you in Egypt.
“Nenda, ukawakusanye wazee wa Israeli, uwaambie, ‘Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Yakobo, alinitokea akaniambia: Nimewatazama, nami nimeona mliyofanyiwa katika Misri.
17 And I have said I will bring up you from [the] affliction of Egypt into [the] land of the Canaanite[s] and the Hittite[s] and the Amorite[s] and the Perizzite[s] and the Hivite[s] and the Jebusite[s] into a land flowing of milk and honey.
Nami nimeahidi kuwapandisha kutoka mateso yenu katika nchi ya Misri, niwapeleke nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, nchi itiririkayo maziwa na asali.’
18 And they will listen to voice your and you will go you and [the] elders of Israel to [the] king of Egypt and you will say to him Yahweh [the] God of the Hebrews he has met with us and therefore let us go please a journey of three days in the wilderness and let us sacrifice to Yahweh God our.
“Wazee wa Israeli watakusikiliza. Kisha wewe na wazee mtakwenda kwa mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania ametutokea. Turuhusu twende safari ya siku tatu huko jangwani kutoa dhabihu kwa Bwana Mungu wetu.’
19 And I I know that not he will permit you [the] king of Egypt to go and not by a hand strong.
Lakini nafahamu kwamba mfalme wa Misri hatawaruhusu kwenda, mpaka mkono wenye nguvu umlazimishe.
20 And I will stretch out hand my and I will strike Egypt with all wonders my which I will do in midst its and after thus he will let go you.
Kwa hiyo nitaunyoosha mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa maajabu yote nitakayofanya miongoni mwao. Baada ya hayo, atawaruhusu mwondoke.
21 And I will give [the] favor of the people this in [the] eyes of Egypt and it will be that you will go! not you will go empty.
“Nami nitawapa hawa watu upendeleo mbele ya Wamisri, kwa hiyo mtakapoondoka nchini hamtaondoka mikono mitupu.
22 And she will ask [each] woman from [female] neighbor her and from [the] [female] sojourner of house her articles of silver and articles of gold and clothes and you will put [them] on sons your and on daughters your and you will plunder Egypt.
Kila mwanamke Mwisraeli atamwomba jirani yake Mmisri na mwanamke yeyote anayeishi nyumbani kwake ampe vyombo vya fedha, dhahabu na nguo, ambavyo mtawavika wana wenu na binti zenu. Hivyo mtawateka nyara Wamisri.”

< Exodus 3 >