< Exodus 13 >

1 And he spoke Yahweh to Moses saying.
Bwana akamwambia Mose,
2 Consecrate to me every firstborn [the] firstborn of every womb among [the] people of Israel among humankind and among the livestock [belongs] to me it.
“Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
3 And he said Moses to the people remember the day this when you went out from Egypt from a house of slaves for with strength of hand he brought out Yahweh you from here and not it will be eaten leaven.
Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
4 This day you [are] about to go out in [the] month of Abib.
Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
5 And it will be that he will bring you Yahweh into [the] land of the Canaanite[s] and the Hittite[s] and the Amorite[s] and the Hivite[s] and the Jebusite[s] which he swore to ancestors your to give to you a land flowing of milk and honey and you will serve the service this in the month this.
Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
6 Seven days you will eat unleavened bread and [will be] on the day seventh a festival of Yahweh.
Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
7 Unleavened bread it will be eaten [the] seven the days and not it will be seen by you leaven and not it will be seen by you leaven in all territory your.
Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
8 And you will tell to child your on the day that saying for sake of what he did Yahweh for me when came out I from Egypt.
Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
9 And it will become for you a sign on hand your and a reminder between eyes your so that may be [the] law of Yahweh in mouth your for by a hand strong he brought out you Yahweh from Egypt.
Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
10 And you will keep the statute this to appointed time its from days days towards.
Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
11 And it will be that he will bring you Yahweh into [the] land of the Canaanite[s] just as he swore to you and to ancestors your and he will give it to you.
“Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
12 And you will dedicate every firstborn of a womb to Yahweh and every firstborn of - [the] offspring of cattle which it will be[long] to you the males [will belong] to Yahweh.
inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
13 And every firstborn of a donkey you will redeem with a sheep and if not you will redeem [it] and you will break neck its and every firstborn of humankind among sons your you will redeem.
Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
14 And it will be that he will ask you son your in future time saying what? [is] this and you will say to him with strength of hand he brought out us Yahweh from Egypt from a house of slaves.
“Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 And it was that he made stubborn Pharaoh to let go us and he killed Yahweh every firstborn in [the] land of Egypt from [the] firstborn of humankind and unto [the] firstborn of livestock there-fore I [am] sacrificing to Yahweh every firstborn of a womb the males and every firstborn of sons my I redeem.
Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
16 And it will become a sign on hand your and marks between eyes your for with strength of hand he brought out us Yahweh from Egypt.
Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
17 And it was when let go Pharaoh the people and not he led them God [the] way of [the] land of [the] Philistines for [was] near it for - he said God lest it should regret the people when see they battle and they will return Egypt towards.
Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
18 And he caused to go around God - the people [the] way of the wilderness [the] sea of reed[s] and arrayed for battle they went up [the] people of Israel from [the] land of Egypt.
Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
19 And he took Moses [the] bones of Joseph with him for certainly he had made swear [the] people of Israel saying certainly he will visit God you and you will take up bones my from here with you.
Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
20 And they set out from Succoth and they encamped at Etham on [the] edge of the wilderness.
Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
21 And Yahweh [was] going before them by day in a pillar of cloud to guide them the journey and night in a pillar of fire to give light to them to go by day and night.
Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
22 Not it departed [the] pillar of cloud by day and [the] pillar of fire night before the people.
Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.

< Exodus 13 >