< Deuteronomy 21 >
1 If it will be found [one] slain in the land which Yahweh God your [is] about to give to you to take possession of it lying in the open country not it is known who? did he strike him.
Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua,
2 And they will go out elders your and judges your and they will measure to the cities which [are] around the [one] slain.
wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani.
3 And it will be the city near to the [one] slain and they will take [the] elders of the city that a heifer of [the] herd which not it has been worked by it which not it has dragged by a yoke.
Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira,
4 And they will bring down [the] elders of the city that the heifer to a wadi ever-flowing which not it is tilled in it and not it is sown and they will break [the] neck of there the heifer in the wadi.
na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo.
5 And they will draw near the priests [the] sons of Levi for them he has chosen Yahweh God your to serve him and to bless in [the] name of Yahweh and on mouth their it will be every dispute and every wound.
Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio.
6 And all [the] elders of the city that near to the [one] slain they will wash hands their over the heifer broken necked in the wadi.
Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde,
7 And they will answer and they will say hands our not (they shed *Q(K)*) the blood this and eyes our not they saw.
nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika.
8 Make atonement for people your Israel which you ransomed O Yahweh and may not you put blood innocent in [the] midst of people your Israel and it will be atoned for for them the blood.
Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho.
9 And you you will remove the blood innocent from midst your for you will do the right in [the] eyes of Yahweh.
Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.
10 If you will go out to war on enemies your and he will give him Yahweh God your in hand your and you will take captive captive[s] his.
Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka,
11 And you will see among the [female] captive[s] a woman beautiful of appearance and you will love her and you will take [her] for yourself to a wife.
kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako.
12 And you will bring her into [the] middle of house your and she will shave head her and she will attend to finger-nails her.
Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake,
13 And she will remove [the] clothing of captivity her from on her and she will dwell in house your and she will weep for father her and mother her a month of days and after thus you will go into her and you will be husband her and she will become of you a wife.
avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako.
14 And it will be if not you delight in her and you will let go her for self her and certainly not you will sell her for money not you will treat as a slave her because that you have humiliated her.
Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.
15 If they will belong to a man two wives the one [is] loved and the one [is] hated and they will bear to him sons the loved [one] and the hated [one] and he will belong the son the firstborn to the hated [wife].
Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda,
16 And it will be on [the] day causes to inherit he sons his [that] which it will belong to him not he will be able to treat as firstborn [the] son the loved [one] on [the] face of [the] son of the hated [one] the firstborn.
wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi.
17 That the firstborn [the] son of the hated [one] he will acknowledge by giving to him a mouth of two in all that it will be found to him for he [is] [the] beginning of manly vigor his [belongs] to him [the] claim of the birthright.
Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.
18 If he will belong to anyone a son stubborn and rebellious not he [is] listening to [the] voice of father his and to [the] voice of mother his (and they will discipline *L(abh)*) him and not he will listen to them.
Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi,
19 And they will seize him father his and mother his and they will bring out him to [the] elders of city his and to [the] gate of place his.
baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake.
20 And they will say to [the] elders of city his son our this [is] stubborn and rebellious not he [is] listening to voice our a glutton and a drunkard.
Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.”
21 And they will stone him all [the] men of city his with stones and he will die and you will remove the evil from midst your and all Israel they will hear and they may fear.
Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.
22 And if it will be in anyone a sin of a sentence of death and he will be put to death and you will hang him on a tree.
Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini,
23 Not it will remain overnight corpse his on the tree for certainly you will bury him on the day that for [is] a curse of God [one who] is hanged and not you will make unclean land your which Yahweh God your [is] about to give to you an inheritance.
kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.