< Deuteronomy 1 >

1 These [are] the words which he spoke Moses to all Israel on [the] other side of the Jordan in the wilderness in the desert plain opposite to Suph between Paran and between Tophel and Laban and Hazeroth and Di Zahab.
Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
2 [is] one [plus] Ten day[s] from Horeb [the] way of [the] mountain of Seir to Kadesh Barnea.
(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
3 And it was in forty year in [the] one [plus] ten month on [day] one of the month he spoke Moses to [the] people of Israel according to all that he had commanded Yahweh him to them.
Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
4 After had defeated he Sihon [the] king of the Amorite[s] who [was] dwelling in Heshbon and Og [the] king of Bashan who [was] dwelling in Ashtaroth in Edrei.
Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
5 On [the] other side of the Jordan in [the] land of Moab he undertook Moses he made clear the law this saying.
Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
6 Yahweh God our he spoke to us at Horeb saying [is] enough for you remaining at the mountain this.
Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
7 Turn - and set out for yourselves and go [the] hill country of the Amorite[s] and to all neighbors its in the desert plain in the hill country and in the Shephelah and in the Negev and on [the] coast of the sea [the] land of the Canaanite[s] and Lebanon to the river great [the] river of Euphrates.
Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
8 See I set before you the land go and take possession of the land which he swore Yahweh to ancestors your to Abraham to Isaac and to Jacob to give to them and to offspring their after them.
Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
9 And I said to you at the time that saying not I am able to alone me to bear you.
Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
10 Yahweh God your he has increased you and here you this day [are] like [the] stars of the heavens for multitude.
Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
11 Yahweh [the] God of ancestors your may he add to you like you a thousand times and may he bless you just as he spoke to you.
Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
12 How? will I bear to alone me burden your and burden your and dispute[s] your.
Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
13 Provide for yourselves men wise and understanding and known to tribes your so I may appoint them chiefs your.
Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
14 And you answered me and you said [is] good the word which you have spoken to do.
Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
15 And I took [the] chiefs of tribes your men wise and known and I appointed them chiefs over you leaders of thousands and leaders of hundreds and leaders of fifties and leaders of tens and officials of tribes your.
Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
16 And I commanded judges your at the time that saying hear between countrymen your and you will judge righteousness between anyone and between countryman his and between sojourner his.
Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
17 Not you will pay regard to faces in judgment as the small as the great you will listen! not you will be afraid of anyone for the judgment [belongs] to God it and the matter which it will be [too] hard for you you will bring near! to me and I will hear it.
Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
18 And I commanded you at the time that all the things which you will do!
Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
19 And we set out from Horeb and we walked all the wilderness great and awesome that which you saw [the] way of [the] hill country of the Amorite[s] just as he had commanded Yahweh God our us and we came to Kadesh Barnea.
Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
20 And I said to you you have come to [the] hill country of the Amorite[s] which Yahweh God our [is] about to give to us.
Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
21 See he sets Yahweh God your before you the land go up take possession of [it] just as he spoke Yahweh [the] God of ancestors your to you may not you be afraid and may not you be dismayed.
Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
22 And you drew near! to me all of you and you said let us send out men before us so they may spy out for us the land so they may bring back us word the way which we will go up on it and the cities which we will go to them.
Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
23 And it was good in view my the thing and I took from you two [plus] ten men a man one to the tribe.
Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
24 And they turned and they went up the hill country towards and they came to [the] wadi of Eshcol and they spied out it.
Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
25 And they took in hand their some of [the] fruit of the land and they brought [it] down to us and they brought back us word and they said [is] good the land which Yahweh God our [is] about to give to us.
Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
26 And not you were willing to go up and you rebelled toward [the] mouth of Yahweh God your.
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
27 And you murmured in tents your and you said in [the] hatred of Yahweh us he brought out us from [the] land of Egypt to give us in [the] hand of the Amorite[s] to destroy us.
Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
28 Where? - [are] we going up countrymen our they have made melt heart our saying [the] people [is] great and lofty more than us [the] cities [are] large and fortified in the heavens and also [the] descendants of [the] Anakites we saw there.
Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
29 And I said to you not you must be terrified! and not you must be afraid! from them.
Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
30 Yahweh God your [is] the [one who] goes before you he he will fight for you according to all that he did with you in Egypt to eyes your.
Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
31 And in the wilderness where you saw that he carried you Yahweh God your just as he carries anyone child his on all the journey which you walked until came you to the place this.
na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
32 And in the thing this not you [were] trusting in Yahweh God your.
Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
33 Who went before you on the journey to seek out for you a place to camp you in the fire - night to show you the way which you will go on it and in the cloud by day.
ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
34 And he heard Yahweh [the] sound of words your and he was angry and he swore an oath saying.
Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
35 If he will see anyone among the men these the generation evil this the land good which I swore to give to ancestors your.
“Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
36 Except Caleb [the] son of Jephunneh he he will see it and to him I will give the land which he has trodden on it and to sons his because that he filled after Yahweh.
isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
37 Also with me he was angry Yahweh on account of you saying also you not you will go there.
Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
38 Joshua ([the] son of *L(abh)*) Nun who stands before you he he will go there towards him encourage for he he will give as an inheritance it Israel.
Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
39 And little one[s] your who you said plunder he will become and children your who not they know this day good and evil they they will go there towards and to them I will give it and they they will take possession of it.
Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
40 And you turn yourselves and set out the wilderness towards [the] way of [the] sea of reed[s].
Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
41 And you answered - and you said to me we have sinned to Yahweh we we will go up and we will fight according to all that he has commanded us Yahweh God our and you girded on everyone [the] weapons of war his and you regarded as easy to go up the hill country towards.
Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
42 And he said Yahweh to me say to them not you must go up and not you must fight for not I [will be] in midst your and not you will be defeated before enemies your.
Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
43 And I spoke to you and not you listened and you rebelled against [the] mouth of Yahweh and you acted presumptuously and you went up the hill country towards.
Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
44 And he came out the Amorite[s] who was dwelling in the hill country that to meet you and they pursued you just as they do bees and they scattered you in Seir to Hormah.
Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
45 And you returned and you wept before Yahweh and not he listened Yahweh to voice your and not he gave ear to you.
Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
46 And you remained at Kadesh days many like the days which you remained.
Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

< Deuteronomy 1 >