< Daniel 5 >

1 Belshazzar king the he made a feast great for nobles his a thousand and before thousand the wine [he was] drinking.
Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao.
2 Belshazzar he said - in [the] taste of wine the to bring [the] vessels of gold and silver which he had brought out Nebuchadnezzar father his from temple the which [was] in Jerusalem so they may drink with them king the and nobles his wives his and concubines his.
Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea.
3 Then they brought [the] vessels of gold which they had brought out from temple the which [was] [the] house of God which [was] in Jerusalem and they drank with them king the and nobles his wives his and concubines his.
Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea.
4 They drank wine the and they praised [the] gods of gold and silver bronze iron wood and stone.
Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.
5 At it moment the (they went forth *Q(K)*) fingers of a hand of a human and [they were] writing before candlestick the on plaster the of [the] wall of palace the of king the and king the [was] seeing [the] palm of hand the which [was] writing.
Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika.
6 Then king the brightness his they changed him and thoughts his they alarmed him and [the] joints of loin[s] his [were] loosened and knees his this [one] to this [one] [were] knocking.
Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.
7 [was] calling King the with power to bring in conjurers the (Chaldeans the *Q(K)*) and astrologers the [was] replying king the and [was] saying - to [the] wise men of Babylon that any person who he will read aloud writing the this and interpretation its he will declare to me purple he will be clothed (and necklace the *Q(k)*) of gold [will be] on neck his and third in kingdom the he will rule.
Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”
8 Then ([were] going in *Q(k)*) all [the] wise men of king the and not [they were] able writing the to read aloud (and interpretation its *Q(K)*) to make known to king the.
Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake.
9 Then king the Belshazzar exceedingly [was] alarmed and brightness his [were] changing on him and nobles his [were] dumbfounded.
Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.
10 Queen the before [the] words of king the and nobles his to [the] house of feast the (she went in *Q(k)*) she replied queen the and she said king O for ever live! may not they alarm you thought[s] your and brightness your may not they be changed.
Malkia aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho!
11 There [is] a man in kingdom your who a spirit of gods holy [is] in him and in [the] days of father your illumination and insight and wisdom like [the] wisdom of gods it was found in him and king the Nebuchadnezzar father your chief of [the] magicians conjurers Chaldeans astrologers he appointed him father your king the.
Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi.
12 As to because that a spirit - extraordinary and understanding and insight an interpreter of dreams and declaring of riddles and loosening of knots it was found in him in Daniel whom king the he made name his Belteshazzar now Daniel let him be summoned and interpretation the he will declare.
Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”
13 Then Daniel he was brought before king the [was] replying king the and [was] saying to Daniel (you *Q(k)*) he [are] Daniel who [is] one of [the] sons of exile the of Judah whom he brought king the father my from Judah.
Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda?
14 And I have heard (concerning you *Q(k)*) that a spirit of gods [is] in you and illumination and insight and wisdom extraordinary it was found in you.
Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee.
15 And now they have been brought before me wise men the conjurers the that writing the this they will read aloud and interpretation its to make known to me and not [they were] able [the] interpretation of matter the to declare.
Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia.
16 And I I have heard (concerning you *Q(k)*) that (you are able *Q(k)*) interpretations to interpret and knots to loosen now if (you will be able *Q(k)*) writing the to read aloud and interpretation its to make known to me purple you will be clothed (and necklace the *Q(k)*) of gold [will be] on neck your and third the in kingdom the you will rule.
Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”
17 Then [was] replying Daniel and [say] saying before king the gifts your for yourself let them be and rewards your to another give! nevertheless writing the I will read aloud to king the and interpretation the I will make known to him.
Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.
18 (You *Q(k)*) king O God (Most High the *Q(k)*) kingdom the and greatness the and honor the and majesty the he gave to Nebuchadnezzar father your.
“Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari.
19 And from greatness the which he gave to him all peoples the nations the and languages the they were (trembling *Q(k)*) and fearing from before him whom he was pleased he was killing and whom he was pleased he was letting live and whom he was pleased he was lifting up and whom he was pleased he was bringing low.
Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha.
20 And as that it rose up heart his and spirit his it grew strong to act presumptuously he was deposed from [the] throne of kingdom his and honor the they removed from him.
Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake.
21 And away from [the] sons of humankind he was chased and heart his - with animal[s] the (they made *Q(K)*) and [was] with wild donkeys the dwelling place his grass like oxen they fed him and from [the] dew of heavens the body his it became wet until that he knew that [was] having mastery God (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of humankind and to whomever whom he will be pleased he will appoint (over it. *Q(K)*)
Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.
22 (And you *Q(k)*) son his O Belshazzar not you have brought low heart your as to because that all this you knew.
“Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.
23 And against [the] lord of heavens the - you have lifted yourself up and vessels the of house his they have brought (before you and you and nobles your *Q(k)*) wives your and concubines your wine [are] drinking with them and [the] gods of silver and gold bronze iron wood and stone who not [are] seeing and not [are] hearing and not [are] knowing you have praised and God the who breath your [is] in hand his and all ways your [are] to him not you have glorified.
Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake.
24 Then from before him it was sent out palm the of hand the and writing the this it was inscribed.
Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.
25 And this [is] writing the which it was inscribed mene mene teqel and pharsin.
“Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa: mene, mene, tekeli na peresi
26 This [is] [the] interpretation of matter the mene he has numbered God kingdom your and he has finished it.
“Hii ndiyo maana ya maneno haya: “Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
27 Teqel you have been weighed in scales the and you have been found lacking.
Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
28 Peres it has been broken in two kingdom your and it has been given to Medes and Persians.
Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
29 Then - he said Belshazzar and they clothed Daniel purple (and necklace the *Q(k)*) of gold [was] on neck his and they made proclamation concerning him that he will be having mastery third the in kingdom the.
Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.
30 On it on night the he was killed Belshazzar king the (Chaldeans the. *Q(k)*)
Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa,
31 And Darius (Median the *Q(K)*) he received kingdom the about a son of years sixty and two.
naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.

< Daniel 5 >