< Daniel 4 >

1 Nebuchadnezzar king the to all peoples the nations the and languages the which ([are] dwelling *Q(k)*) in all earth the peace your may it increase.
Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
2 Signs the and wonders the which he has done with me God (Most High the *Q(k)*) it seemed good before me to declare.
Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
3 [are] signs His how much! great and [are] wonders his how much! strong kingdom his [is] a kingdom of perpetuity and dominion his [is] with generation and generation.
Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
4 I Nebuchadnezzar at ease I was in house my and flourishing in palace my.
Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
5 A dream I saw and it made afraid me and imaginings on bed my and [the] visions of head my they alarmed me.
Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
6 And from me it was made a decree to bring in before me all [the] wise men of Babylon that [the] interpretation of dream the they will make known to me.
Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
7 Then ([were] going in *Q(k)*) magicians the conjurers the (Chaldeans the *Q(K)*) and astrologers the and dream the [was] saying I before them and interpretation its not [they were] making known to me.
Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
8 And until at last he came in before me Daniel who name his [is] Belteshazzar like [the] name of god my and who a spirit of gods holy [is] in him and dream the before him I said.
Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
9 O Belteshazzar [the] chief of magicians the whom - I I know that a spirit of gods holy [is] in you and any secret not [is] oppressing you [the] visions of dream my which I saw and interpretation its tell!
Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
10 And [the] visions of head my on bed my seeing I was and lo! a tree in [the] midst of land the and height its [was] great.
Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
11 It grew great tree the and it grew strong and height its it reached to heavens the and [the] sight of it [was] to [the] end of all land the.
Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
12 Foliage its [was] beautiful and fruit its [was] plentiful and food for all [was] on it under it it had shade - [the] animal[s] of field the and in branches its (they nested *Q(K)*) [the] birds of heavens the and from it it fed all flesh.
Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
13 Seeing I was in [the] visions of head my on bed my and lo! a watcher and a holy [one] from heavens the [was] coming down.
“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
14 [he was] proclaiming With power and as follows [he was] saying cut down! tree the and cut off! branches its strip off! foliage its and scatter! fruit its let it flee animal[s] the from under it and birds the from branches its.
Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
15 Nevertheless [the] stump of roots its in ground the leave! and with a fetter of iron and bronze in grass the of field the and with [the] dew of heavens the let it become wet and [be] with animal[s] the portion its in [the] grass of earth the.
Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
16 Heart its away from (human the *Q(k)*) let it be changed and [the] heart of an animal let it be given to it and seven times let them pass over it.
Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
17 [is] by [the] decree of Watchers command the and [is by the] word of holy [ones] affair the to [the] cause that they will know living [people] the that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of (human the *Q(k)*) and to whomever whom he will be pleased he will give it and a lowly [one] of humankind he will set up (over it. *Q(k)*)
“‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
18 This dream the I saw I king the Nebuchadnezzar (and you *Q(k)*) O Belteshazzar interpretation its - tell! as to because that - all [the] wise men of kingdom my not [are] able interpretation the to make known to me (and you *Q(k)*) [are] able who a spirit of gods holy [is] in you.
“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
19 Then Daniel who name his [was] Belteshazzar he was appalled about a moment one and thoughts his they alarmed him [was] replying king the and [was] saying O Belteshazzar dream the and interpretation its may not it alarm you [was] replying Belteshazzar and [was] saying (O lord my *Q(k)*) dream the ([be] for enemy your *Q(K)*) and interpretation its ([be] for adversaries your. *Q(k)*)
Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
20 Tree the which you saw which it grew great and it grew strong and height its it reached to heavens the and [the] sight of it [was] to all land the.
Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
21 And foliage its [was] beautiful and fruit its [was] plentiful and food for all [was] on it under it it dwelt [the] animal[s] of field the and in branches its they dwelt [the] birds of heavens the.
ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
22 ([is] you *Q(k)*) It king O who you have grown great and you have grown strong and greatness your it has grown great and it has reached to heavens the and dominion your [is] to [the] end earth the.
Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
23 And that he saw king the a watcher and a holy [one] coming down - from heavens the and saying cut down! tree the and destroy it nevertheless [the] stump of roots its in ground the leave! and with a fetter of iron and bronze in grass the of field the and with [the] dew of heavens the let it become wet and [be] with [the] animal[s] of field the portion its until that seven times they will pass over it.
“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
24 This [is] interpretation the king O and [is] [the] decree of (Most High the *Q(k)*) it which it has reached to (lord my *Q(k)*) king the.
“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
25 And you [they will be] chasing away from humankind and with [the] animal[s] of field the it will be dwelling place your and grass like oxen - to you they will feed and from [the] dew of heavens the you [they will be] making wet and seven times they will pass (over you *Q(k)*) until that you will know that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of humankind and to whomever whom he will be pleased he will give it.
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
26 And that they said to leave [the] stump of roots its of tree the kingdom your to you [will be] enduring from that you will know that [are] having mastery heavens the.
Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
27 Therefore king O advice my let it be acceptable (to you *Q(k)*) (and sin your *Q(K)*) by right doing break off! and iniquities your by showing mercy to poor people whether it will be a prolonging of prosperity your.
Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
28 Everything it came on Nebuchadnezzar king the.
Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
29 To [the] end of months two [plus] ten on [the] palace of kingdom the of Babylon walking about he was.
Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
30 [was] replying King the and [was] saying ¿ not [is] this it Babylon great which I I built it to a house of a kingdom by [the] strength of power my and for [the] honor of majesty my.
alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
31 Still word the [was] in [the] mouth of king the a voice from heavens the it fell to you [they are] saying O Nebuchadnezzar king the kingdom the it has passed away from you.
Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
32 And away from humankind you [they are] about to chase and [will be] with [the] animal[s] of field the dwelling place your grass like oxen to you they will feed and seven times they will pass (over you *Q(k)*) until that you will know that [is] having mastery (Most High the *Q(k)*) over [the] kingdom of humankind and to whomever whom he will be pleased he will give it.
Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
33 At it moment the word the it was fulfilled on Nebuchadnezzar and away from humankind he was chased and grass like oxen he ate and from [the] dew of heavens the body his it became wet until that hair his like eagles it grew long and nails his [were] like birds.
Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
34 And to [the] end of days the I Nebuchadnezzar eye my - to heavens the I lifted and understanding my on me it returned (and Most High the *Q(k)*) I blessed and [the] [one] living of perpetuity I praised and I glorified that dominion his [is] a dominion of perpetuity and kingdom his [is] with generation and generation.
Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
35 And all ([the] inhabitants of *Q(k)*) earth the [are] as not considered and as pleases he [he is] doing with [the] army of heavens the (and [the] inhabitants of *Q(k)*) earth the and not there [is] who he will strike on hand his so he may say to him what? have you done.
Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
36 At it time the understanding my - it returned to me and to [the] honor of kingdom my majesty my and splendor my it returned to me and me counselors my and nobles my they sought and over kingdom my it was established and greatness surpassing it was added to me.
Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
37 Now I Nebuchadnezzar [am] praising and [am] lifting up and [am] glorifying [the] king of heavens the who all deeds his [are] truth and ways his [are] justice and [those] who [are] walking in pride [he is] able to bring low.
Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.

< Daniel 4 >