< Colossians 4 >
1 you who [are] Masters, that which [is] righteous and that which [is] equal to the slaves do give knowing that also you yourselves have a Master in (heaven. *N(k)O*)
Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua ya kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 In prayer do continue steadfastly watching in it with thanksgiving;
Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru.
3 praying at the same time also for us that God may open to us a door for the word to declare the mystery of Christ, on account of which also I have been bound,
Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.
4 so that I may make clear it as it behooves me to speak.
Ombeni ili nipate kuitangaza Injili kwa udhahiri kama ipasavyo kunena.
5 In wisdom do walk toward those outside the time redeeming.
Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
6 [Let] the speech of you [be] always in grace, with salt seasoned, to know how it behooves you one each to answer.
Maneno yenu yawe yamejaa neema siku zote, yanayofaa, ili mjue jinsi iwapasavyo na inavyofaa kumjibu kila mtu.
7 The [things] concerning me myself all will make known to you Tychicus the beloved brother and faithful servant and fellow bond-servant in [the] Lord,
Tikiko atawaambia habari zangu zote. Yeye ni ndugu mpendwa, mtendakazi mwaminifu na mtumishi mwenzangu katika Bwana.
8 whom I sent to you for this very purpose that (you may know *N(K)(O)*) the [things] concerning (us *N(K)O*) and he may encourage the hearts of you,
Nimemtuma kwenu kwa madhumuni haya ili mpate kufahamu hali yetu, na pia awatie moyo.
9 with Onesimus the faithful and beloved brother, who is [one] of you; All things to you they will make known here.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa na mwaminifu, ambaye ni mmoja wenu. Watawaambia mambo yote yanayotendeka hapa kwetu.
10 Greets you Aristarchus the fellow prisoner of mine and Mark the cousin of Barnabas, concerning whom you have received instructions: if he shall come to you, do welcome him;
Aristarko aliye mfungwa pamoja nami anawasalimu, vivyo hivyo Marko, binamu yake Barnaba. (Mmeshapata maagizo yanayomhusu; akija kwenu, mpokeeni.)
11 and also Jesus who is being named Justus, those being among [the] circumcision these only fellow workers for the kingdom of God, who have been to me a comfort.
Yesu, yeye aitwaye Yusto, pia anawasalimu. Hawa peke yao ndio Wayahudi miongoni mwa watendakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, nao wamekuwa faraja kwangu.
12 Greets you Epaphras who [is] [one] of you, a servant of Christ (Jesus, *NO*) always struggling for you in the prayers, so that (you may be stood *N(k)O*) mature and (fully complete *N(k)O*) in all [the] will of God.
Epafra, ambaye ni mmoja wenu na mtumishi wa Kristo Yesu, anawasalimu. Yeye siku zote anawaombea kwa bidii kwamba msimame imara katika mapenzi yote ya Mungu, mkiwa wakamilifu na thabiti.
13 I bear witness for to him that he has great (labour *N(K)O*) for you and those in Laodicea and [those] of them in Hiera polis.
Ninashuhudia kumhusu kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, na kwa ajili ya ndugu wa Laodikia na wale wa Hierapoli.
14 Greets you Luke the physician beloved and also Demas.
Rafiki yetu mpenzi Luka yule tabibu, pamoja na Dema, wanawasalimu.
15 do greet the in Laodicea brothers and also (Nympha *N(K)O*) and the in house (of her *N(K)(o)*) church.
Wasalimuni ndugu wote wa Laodikia, na pia Nimfa, pamoja na kanisa linalokutana katika nyumba yake.
16 And when may be read among you the letter, do cause that also in the of [the] Laodiceans church it may be read, and the [one] from Laodicea that also you yourselves may read.
Baada ya barua hii kusomwa kwenu, hakikisheni kwamba inasomwa pia katika kanisa la Walaodikia. Nanyi pia msome barua inayotoka Laodikia.
17 And do say to Archippus; do take heed to the ministry that you have received in [the] Lord, that it you may fulfill.
Mwambieni Arkipo hivi: “Hakikisha kuwa unakamilisha ile huduma uliyopokea katika Bwana.”
18 The greeting in my own hand — by Paul. do remember my chains. Grace [be] with you (Amen. *KO*) (to Colossian it was written from Rome through Tychicus and Onesimus. *K*)
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni minyororo yangu. Neema iwe nanyi. Amen.