< Acts 26 >
1 Agrippa then to Paul was saying; It is permitted you (for *N(k)O*) yourself to speak. Then Paul having stretched out the hand was presenting a defense:
Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
2 Concerning all of which I am accused by [the] Jews, King Agrippa, I have esteemed myself fortunate before you being about today to present a defense;
“Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
3 Especially acquainted being you with all the of [the] Jews (customs *NK(o)*) and also controversies. therefore I implore (you *k*) patiently to hear me.
hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
4 The indeed then manner of life of mine which [is] from youth from [its] beginning having been among the nation of mine in (also *no*) Jerusalem know all the Jews
“Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
5 knowing me from the first, if they may be willing to testify that according to the strictest sect of our own religion I lived [as] a Pharisee;
Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
6 And now for [the] hope of the (to *N(k)O*) the fathers of us promise having been made by God I have stood being judged,
Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
7 to which the twelve tribes of us in earnestness night and day serving they hope to attain, concerning which hope I am accused (Agrippa *K*) by (the *k*) Jews, O king,
Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
8 Why incredible is it judged by you if God [the] dead raises?
Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
9 I myself indeed therefore thought in myself to the name of Jesus of Nazareth needing many things contrary to do,
“Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
10 which also I did in Jerusalem and many (also *no*) of the saints I myself (in *no*) prisons locked up the from the chief priests authority having received, when were being executed then they I cast against [them] a vote;
Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
11 And in all the synagogues often punishing them I was compelling [them] to blaspheme, Excessively then being furious against them I was persecuting [them] as far as even to foreign cities.
Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
12 during which (and *k*) journeying to Damascus with [the] authority and commission which [is] (from *k*) the chief priests
“Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
13 At day mid on the road I saw, O king, from heaven above the brightness of the sun having shone around me a light and those with me myself journeying.
Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
14 All (and *N(k)O*) when were falling down we to the ground I heard a voice (saying *N(k)O*) to me (and saying *k*) in the Hebrew language; Saul Saul, why Me persecute you? [It is] hard for you against [the] goads to kick.
Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
15 I myself then said; Who are You Lord? And (the Lord *no*) said; I myself am Jesus whom you yourself are persecuting.
“Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
16 But do rise up and do stand on the feet of you; to this [purpose] for I have appeared to you to appoint you a servant and a witness of that which both you have seen (of Me *NO*) of the things in which then I will appear to you,
Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
17 delivering you out from the people and (from *no*) the Gentiles, to whom (I myself *N(K)O*) am sending you
Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
18 to open eyes of them, that (to turn *NK(o)*) from darkness to light and from the power of Satan to God, [that] to receive they forgiveness of sins and [an] inheritance among those sanctified by faith which [is] in Me myself.
uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
19 So then, O king Agrippa, not I was disobedient to the heavenly vision,
“Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
20 but to those in Damascus first (both *no*) also in Jerusalem (into *k*) all both the region of Judea, and to the Gentiles (I was declaring *N(k)O*) to repent and to turn to God worthy of repentance works doing.
bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
21 On account of these things me (the *k*) Jews having seized (being *n*) in the temple they were attempting to kill.
Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
22 Help therefore having obtained (from *N(k)O*) God unto day this I have stood (bearing witness *N(k)O*) to small both and to great, no [thing] other saying than what both the prophets said was about to happen and Moses,
Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
23 that would suffer the Christ, as first through resurrection from [the] dead light He is about to preach (to both *no*) our people and to the Gentiles.
kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
24 These things now when he is presenting a defense Festus in a loud voice (said; *N(k)O*) You are insane Paul! The great of you learning to insanity turns [you]!
Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
25 But (Paul; *no*) Not I am insane says most excellent Festus, but of truth and sobriety declarations I utter.
Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
26 Understands for concerning these things the king to whom also using boldness I speak; Hiding for him any of these things not I am persuaded no [thing]; not for is in a corner done of these things.
Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
27 Believe you, King Agrippa, in the prophets? I know that you believe.
Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
28 Then Agrippa to Paul (was saying: *k*) Within so little [time] me you [seek to] persuade a Christian (to become! *N(k)O*)
Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
29 And Paul (said; *k*) I would wish may God both in a little and in (much *N(k)O*) not only you but also all those hearing me this day to become such as also I myself am except chains these.
Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
30 (and these things when was speaking he *K*) rose up (then *no*) the king and the governor and Bernice and those sitting with them;
Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
31 and having withdrawn they were speaking to one another saying that No [thing] of death or of chains worthy (any *NO*) is doing man this.
Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
32 Agrippa then to Festus was saying; to have been released was able man this, only unless he had appealed to Caesar.
Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”