< 2 Samuel 10 >

1 And it was after thus and he died [the] king of [the] people of Ammon and he reigned Hanun son his in place his.
Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
2 And he said David I will do covenant loyalty - with Hanun [the] son of Nahash just as he did father his with me covenant loyalty and he sent David to comfort him by [the] hand of servants his concerning father his and they came [the] servants of David [the] land of [the] people of Ammon.
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
3 And they said [the] leaders of [the] people of Ammon to Hanun lord their ¿ honoring [is] David father your in view your for he has sent to you comforters ¿ not in order to explore the city and to spy on it and to overthrow it has he sent David servants his to you.
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
4 And he took Hanun [the] servants of David and he shaved half of beard their and he cut off robes their at the middle to buttocks their and he sent away them.
Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 And people told to David and he sent to meet them for they were the men humiliated very and he said the king remain at Jericho until it will grow back beard your and you will return.
Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
6 And they saw [the] people of Ammon that they had made themselves odious with David and they sent [the] people of Ammon and they hired Aram Beth Rehob and Aram Zobah twenty thousand foot soldier[s] and [the] king of Maacah one thousand man and [the] man of Tob two [plus] ten thousand man.
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
7 And he heard David and he sent Joab and all the army the warriors.
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
8 And they went out [the] people of Ammon and they deployed battle [the] entrance of the gate and Aram Zobah and Rehob and [the] man of Tob and Maacah to alone them [were] in the open country.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
9 And he saw Joab that it was against him [the] face of the battle from before and from behind and he chose some of all [the] chosen [men] (of Israel *Q(K)*) and he deployed [them] to meet Aram.
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
10 And [the] rest of the people he put in [the] hand of Abishai brother his and he deployed [them] to meet [the] people of Ammon.
Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
11 And he said if it will be [too] strong Aram for me and you will become of me deliverance and if [the] people of Ammon they will be [too] strong for you and I will come to deliver you.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
12 Be strong so we may show ourselves strong for people our and for [the] cities of God our and Yahweh he will do the good in view his.
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
13 And he drew near Joab and the people which [was] with him for battle in Aram and they fled from before him.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
14 And [the] people of Ammon they saw that it had fled Aram and they fled from before Abishai and they went the city and he returned Joab from on [the] people of Ammon and he came Jerusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
15 And it saw Aram that it was defeated before Israel and they gathered themselves together.
Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
16 And he sent Hadadezer and he brought out Aram which [was] from [the] other side of the River and they came Helam and Shobach [the] commander of [the] army of Hadadezer [was] before them.
Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
17 And it was told to David. And he gathered all Israel and he passed over the Jordan and he came Helam towards and they deployed Aram to meet David and they did battle with him.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
18 And it fled Aram from before Israel and he killed David of Aram seven hundred charioteer[s] and forty thousand horsemen and Shobach [the] commander of army its he struck down and he died there.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
19 And they saw all the kings [the] servants of Hadadezer that they were defeated before Israel and they made peace with Israel and they served them and they were afraid Aram to deliver again [the] people of Ammon.
Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.

< 2 Samuel 10 >