< 2 Kings 25 >

1 And it was in [the] year ninth of reigning his in the month tenth on the ten of the month he came Nebuchadnezzar [the] king of Babylon he and all army his on Jerusalem and he encamped on it and they built on it a siege-wall all around.
Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
2 And it came the city in state of siege until one [plus] ten year of the king Zedekiah.
Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
3 (In the month fourth *X*) on [day] nine of the month and it was severe the famine in the city and not it belonged food to [the] people of the land.
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
4 And it was broken into the city and all [the] men of war - this night [the] way of [the] gate - between the two walls which [was] at [the] garden of the king and [the] Chaldeans [were] on the city all around and he went [the] direction of the Arabah.
Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
5 And they pursued [the] army of [the] Chaldeans after the king and they overtook him in [the] plains of Jericho and all army his they were scattered from with him.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
6 And they seized the king and they brought up him to [the] king of Babylon Riblah towards and they spoke with him judgment.
Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
7 And [the] sons of Zedekiah they slaughtered to eyes his and [the] eyes of Zedekiah he made blind and he bound him with bronze fetters and he brought him Babylon.
Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
8 And in the month fifth on [day] seven of the month it [was] year nine-teen year of the king Nebuchadnezzar [the] king of Babylon he came Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards [the] servant of [the] king of Babylon Jerusalem.
Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
9 And he burned [the] house of Yahweh and [the] house of the king and all [the] houses of Jerusalem and every house of a great [person] he burned with fire.
Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
10 And [the] walls of Jerusalem all around they broke down all [the] army of [the] Chaldeans who [was the] chief of [the] bodyguards.
Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
11 And [the] rest of the people which remained in the city and those [who] fell who they fell on the king of Babylon and [the] rest of the multitude he took into exile Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards.
Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
12 And some of [the] poor people of the land he left behind [the] chief of [the] bodyguards to vinedressers and to ploughmen.
Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
13 And [the] pillars of bronze which [were] [the] house of Yahweh and the stands and [the] sea of bronze which [was] in [the] house of Yahweh they broke [the] Chaldeans and they carried bronze their Babylon towards.
Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
14 And the pots and the shovels and the snuffers and the pans and all [the] articles of bronze which people served with them they took.
Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
15 And the fire-pans and the bowls which [were] gold gold and which [were] silver silver he took [the] chief of [the] bodyguards.
Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
16 The pillars - two the sea one and the stands which he had made Solomon for [the] house of Yahweh not it belonged weight to [the] bronze of all the articles these.
Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
17 [was] eight-Teen cubit[s] [the] height of - the pillar one and a capital [was] on it - bronze and [the] height of the capital [was] three (cubits *Q(K)*) and a network and pomegranates [were] on the capital all around everything [was] bronze and like these [things] [belonged] to the pillar second with the network.
Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
18 And he took [the] chief of [the] bodyguards Seraiah [the] priest of the head and Zephaniah a priest second and [the] three [the] keepers of the threshold.
Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
19 And from the city he took a court-official one who he [was] overseer - over [the] men of war and five men from [those who] saw [the] face of the king who they were found in the city and the scribe [the] commander of the army who mustered [the] people of the land and sixty man from [the] people of the land who were found in the city.
Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
20 And he took them Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards and he brought them to [the] king of Babylon Riblah towards.
Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
21 And he struck down them [the] king of Babylon and he put to death them at Riblah in [the] land of Hamath and it went into exile Judah from on land its.
Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
22 And the people who remained in [the] land of Judah whom he left behind Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and he appointed over them Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan.
Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
23 And they heard all [the] commanders of the armies they and the men that he had appointed [the] king of Babylon Gedaliah and they came to Gedaliah Mizpah and Ishmael [the] son of Nethaniah and Johanan [the] son of Kareah and Seraiah [the] son of Tanhumeth the Netophathite and Jaazaniah [the] son of the Maacathite they and men their.
Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
24 And he swore an oath to them Gedaliah and to men their and he said to them may not you be afraid from [the] servants of the Chaldeans dwell in the land and serve [the] king of Babylon so it may go well for you.
Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
25 And it was - in the month seventh he came Ishmael [the] son of Nethaniah [the] son of Elishama one of [the] offspring of royalty and ten men with him and they struck down Gedaliah and he died and the Jews and the Chaldeans who they were with him at Mizpah.
Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
26 And they arose all the people from [the] small and unto [the] great and [the] commanders of the armies and they went Egypt for they were afraid of [the] Chaldeans.
Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
27 And it was in thirty and seven year of [the] exile of Jehoiachin [the] king of Judah in two [plus] ten month on [day] twenty and seven of the month he lifted up Evil-Merodach [the] king of Babylon in [the] year became king he [the] head of Jehoiachin [the] king of Judah from [the] house of imprisonment.
Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
28 And he spoke with him good and he set throne his above [the] throne of the kings who [were] with him in Babylon.
Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
29 And he changed [the] clothes of imprisonment his and he ate bread continually before him all [the] days of life his.
Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
30 And allowance his an allowance of continuity it was given to him from with the king [the] matter of a day in day its all [the] days of life his.
na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.

< 2 Kings 25 >