< 2 Kings 24 >

1 In days his he came up Nebuchadnezzar [the] king of Babylon and he was of him Jehoiakim a subject three years and he turned back and he rebelled against him.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 And he sent Yahweh - on him [the] marauding bands of [the] Chaldeans and [the] marauding bands of Aram and - [the] marauding bands of Moab and [the] marauding bands of [the] people of Ammon and he sent them on Judah to destroy it according to [the] word of Yahweh which he had spoken by [the] hand of servants his the prophets.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 Surely - on [the] mouth of Yahweh it happened in Judah to remove [it] from on face his for [the] sins of Manasseh according to all that he had done.
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 And also [the] blood of the innocent which he had shed and he filled Jerusalem blood innocent and not he was willing Yahweh to forgive.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 And [the] rest of [the] matters of Jehoiakim and all that he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 And he lay down Jehoiakim with ancestors his and he became king Jehoiachin son his in place of him.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 And not he repeated again [the] king of Egypt to come out from own land his for he had taken [the] king of Babylon from [the] wadi of Egypt to [the] river of Euphrates all that it had belonged to [the] king of Egypt.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 [was] a son of Eight-teen year[s] Jehoiachin when became king he and three months he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Nehushta [the] daughter of Elnathan from Jerusalem.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to all that he had done father his.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 At the time that (they went up *Q(K)*) [the] servants of Nebuchadnezzar [the] king of Babylon Jerusalem and it came the city in state of siege.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 And he came Nebuchadnezzar [the] king of Babylon to the city and servants his [were] laying siege on it.
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 And he went out Jehoiachin [the] king of Judah to [the] king of Babylon he and mother his and servants his and officials his and court-officials his and he took him [the] king of Babylon in year eight of reigning his.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 And he brought out from there all [the] treasures of [the] house of Yahweh and [the] treasures of [the] house of the king and he cut up all [the] articles of gold which he had made Solomon [the] king of Israel for [the] temple of Yahweh just as he had spoken Yahweh.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 And he took into exile all Jerusalem and all the officials and - all [the] mighty [men] of strength (ten *Q(K)*) thousand exile[s] and every craftsman and smith not anyone was left except [the] poor people of [the] people of the land.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 And he took into exile Jehoiachin Babylon towards and [the] mother of the king and [the] wives of the king and court-officials his and ([the] leaders of *Q(K)*) the land he led away exile[s] from Jerusalem Babylon towards.
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 And all [the] men of strength seven thousand and the craftsman and the smith one thousand everyone warriors makers of war and he brought them [the] king of Babylon exile[s] Babylon towards.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 And he made king [the] king of Babylon Mattaniah uncle his in place of him and he changed name his Zedekiah.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 [was] a son of Twenty and one year[s] Zedekiah when became king he and one [plus] ten year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his ([was] Hamutal *Q(K)*) [the] daughter of Jeremiah from Libnah.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to all that he had done Jehoiakim.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 For - on [the] anger of Yahweh it happened in Jerusalem and in Judah until threw he them from on face his and he rebelled Zedekiah against [the] king of Babylon.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

< 2 Kings 24 >