< 2 Corinthians 12 >
1 To boast (it behooves [me], *N(K)O*) not (is it profitable indeed, *N(K)O*) I will go on (however *N(k)O*) to visions and revelations of [the] Lord.
Yanipasa nijisifu, ingawa haifaidi kitu. Nitaenda kwenye maono na ufunuo kutoka kwa Bwana.
2 I know a man in Christ ago years fourteen — whether in [the] body not I know, or out of the body not I know, God knows — having been caught up such a man until [the] third heaven.
Namjua mtu mmoja katika Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alichukuliwa juu hadi mbingu ya tatu. Kama ni katika mwili au nje ya mwili, sijui, Mungu ajua.
3 And I know such a man — whether in [the] body or (out of *N(k)O*) the body, not I know, God knows —
Nami najua ya kwamba mtu huyu, kwamba ni katika mwili au nje ya mwili mimi sijui, lakini Mungu ajua,
4 that he was caught up into Paradise and he heard inexpressible declaration which not being permitted to man to speak.
alinyakuliwa hadi Paradiso. Huko alisikia mambo yasiyoelezeka, mambo ambayo binadamu hana ruhusa ya kuyasimulia.
5 Concerning such a man I will boast, concerning however myself not I will boast only except in the weaknesses (of mine; *K*)
Nitajisifu kwa ajili ya mtu kama huyo, lakini sitajisifu kuhusu mimi mwenyewe ila mimi nitajisifia udhaifu wangu.
6 If for I shall desire to boast, not I will be a fool; [the] truth for I will be speaking; I refrain however lest anyone to me myself may credit more than what he sees in me, or hears anything of me
Hata kama ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga, kwa maana nitakuwa nasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu yeyote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.
7 and the by surpassingness of the revelations. (Therefore *NO*) that not I may become conceited, was given to me a thorn in [my] flesh, a messenger of Satan that me he may buffet so that not I may become conceited.
Ili kunizuia nisijivune kwa sababu ya ufunuo huu mkuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mjumbe wa Shetani, ili anitese.
8 For this three times the Lord I begged that it may depart from me.
Kwa habari ya jambo hili nilimsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu.
9 And He has said to me; Suffices you the grace of Mine; the for power (of mine *K*) in weakness (is finished. *N(k)O*) Most gladly therefore rather will I boast in the weaknesses of mine, so that may rest upon me myself the power of Christ.
Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uweza wangu hukamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
10 Therefore I take pleasure in weaknesses, in insults, in hardships, in persecutions (and *N(k)O*) difficulties for Christ; when for I may be weak then strong I am.
Hii ndiyo sababu, kwa ajili ya Kristo, nafurahia udhaifu, katika kutukanwa, katika taabu, katika mateso na katika shida, kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo nina nguvu.
11 I have become a fool (boasting; *K*) you yourselves me compelled. I myself for was being obliged by you to have been commended; [In] no[thing] for was I inferior to those most eminent most eminent apostles, if even no [thing] I am.
Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ilinipasa kusifiwa na ninyi, kwa sababu mimi si dhalili kuliko wale “mitume walio bora,” ingawa mimi si kitu.
12 The indeed signs of the apostle were performed among you in all perseverance, (in *k*) signs (both *no*) and in wonders and in miracles.
Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani, ishara, miujiza na maajabu, yalifanywa miongoni mwenu kwa saburi nyingi.
13 In what for is it that you were inferior beyond the rest [of the] churches, only except that myself I myself not did burden you? do forgive me wrong this!
Je, ninyi ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila tu kwamba mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili!
14 Behold third time (this *no*) ready I am to come to you and not I will burden (you; *k*) not for I seek what [is] yours but you. Not for ought the children for the parents to treasure up but the parents for the children;
Sasa niko tayari kuja kwenu kwa mara hii ya tatu, nami sitawalemea, kwa sababu sitahitaji chochote chenu, ila ninawahitaji ninyi, kwa kuwa hata hivyo watoto hawaweki akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi huweka akiba kwa ajili ya watoto wao.
15 I myself now most gladly will spend and I will be utterly spent for the souls of you, If (even *k*) more abundantly you (loving *NK(o)*) (less *N(k)O*) I am loved!
Hivyo nitafurahi kutumia kila kitu nilicho nacho kwa ajili yenu, hata mwili wangu pia. Hata ingawa inaonekana ninavyozidi kuwapenda, ndivyo upendo wenu kwangu unavyopungua.
16 it should be however, I myself not did burden you; but being crafty by trickery you I caught.
Iwe iwavyo, kwa vyovyote vile mimi sikuwalemea. Lakini kwa mimi kuwa mwerevu naliwapata.
17 Surely not any of whom I have sent to you, through him did I exploit you?
Je, nilijipatia faida kwa kumtumia mtu yeyote niliyemtuma kwenu?
18 I urged Titus [to go] and sent with [him] the brother; surely not ever did exploit you Titus? Surely in the same spirit did we walk? Not in the same steps?
Nilimshawishi Tito aje kwenu, nami nilimtuma pamoja na ndugu yetu. Je, Tito aliwatumia ninyi ili kujipatia faida? Je, hatuenendi kwa roho moja, na hatuchukui hatua zile zile?
19 (Previously *N(K)O*) you have been thinking that to you we are presenting a defense. (before *N(k)O*) (*k*) God in Christ we speak. but all things, beloved, for your edification.
Je, mmekuwa mkifikiri kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu? Sisi tumekuwa tukinena mbele za Mungu kama wale walio katika Kristo. Na chochote tufanyacho, ndugu wapendwa, ni kwa ajili ya kuwatia nguvu.
20 I fear for lest perhaps having come not such as I wish I may find you, and I myself and I myself may be found by you such as not you do wish, lest perhaps (a quarrel, jealousy, *N(k)O*) anger, contentions slander, gossip, conceit, disorder,
Kwa kuwa nina hofu ya kwamba nitakapokuja naweza kuwakuta nisivyotaka, nanyi mkanikuta msivyotaka. Nina hofu kwamba panaweza kuwa na ugomvi, wivu, ghadhabu, fitina, masingizio, masengenyo, majivuno na machafuko.
21 lest again (when was coming *N(k)O*) (I *no*) (he may humble *NK(o)*) me the God, of mine before you, and I may mourn over many of those having sinned before and not having repented of the impurity and of sexual immorality and of sensuality that they have practiced.
Nina hofu kwamba nitakapokuja tena kwenu, Mungu wangu atanidhili mbele yenu, nami nitasikitishwa na wengi waliotenda dhambi mbeleni, na wala hawajatubu kwa uchafu wao, uasherati, na ufisadi walioushiriki.