< 1 Samuel 27 >

1 And he said David to heart his now I will be swept away a day one by [the] hand of Saul not [belongs] to me good for really I will escape - to [the] land of [the] Philistines and he will desist from me Saul to seek me again in all [the] territory of Israel and I will be delivered from hand his.
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 And he arose David and he passed over he and six hundred man who [were] with him to Achish [the] son of Maoch [the] king of Gath.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 And he dwelt David with Achish in Gath he and men his each one and household his David and [the] two wives his Ahinoam the Jezreelite [woman] and Abigail [the] wife of Nabal the Carmelite [woman].
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 And it was told to Saul that he had fled David Gath and not (he repeated *Q(K)*) again to seek him.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 And he said David to Achish if please I have found favor in view your let people give to me a place in one of [the] cities of the field so I may dwell there and why? will he dwell servant your in [the] city of royalty with you.
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 And he gave to him Achish on the day that Ziklag therefore it has belonged Ziklag to [the] kings of Judah until the day this.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 And it was [the] number of the days which he dwelt David in [the] region of [the] Philistines days and four months.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 And he went up David and men his and they made raids against the Geshurite[s] (and the Gizrite[s] *Q(K)*) and the Amalekite[s] for they [were] dwelling the land which [is] from antiquity coming you Shur towards and to [the] land of Egypt.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 And he struck David the land and not he let live a man and a woman and he took sheep and cattle and donkeys and camels and clothes and he returned and he went to Achish.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 And he said Achish against [where] did you make a raid this day and he said David on [the] Negev of Judah and on [the] Negev of the Jerahmeelite[s] and against [the] Negev of the Kenite[s].
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 And a man and a woman not he let live David to bring Gath saying lest they should tell on us saying thus he has done David and [is] thus practice his all the days which he has dwelt in [the] region of [the] Philistines.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 And he trusted Achish in David saying certainly he has become odious among people his among Israel and he will become of me a servant of perpetuity.
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

< 1 Samuel 27 >