< 1 Samuel 2 >

1 And she prayed Hannah and she said it rejoices heart my in Yahweh it is exalted horn my in Yahweh it has opened wide mouth my on enemies my for I rejoiced in deliverance your.
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There not [is] a holy [one] like Yahweh for there not [is] except you and there not [is] a rock like God our.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 May not you multiply you will speak haughty haughty it goes out arrogance from mouth your for [is] a God of knowledge Yahweh (and by him *Q(K)*) they are measured deeds.
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 [the] bow of Warriors [are] shattered and [those who] stumble they gird on strength.
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 Satisfied [people] for food they hire themselves out and hungry [people] they cease to a barren [woman] she bears seven [children] and [a woman] many of sons she languishes.
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 Yahweh [is] killing and [is] restoring to life [he is] bringing down Sheol and he has brought up. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 Yahweh [is] making poor and [is] making rich [he is] bringing low also [is] exalting.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 [he is] raising up From [the] dust [the] poor from [the] ash heap he lifts up [the] needy to cause [them] to dwell with noble [people] and a throne of honor he makes inherit them for [belong] to Yahweh [the] pillars of [the] earth and he set on them [the] world.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 [the] feet of (Faithful [people] his *Q(K)*) he will protect and wicked [people] in the darkness they will be silenced for not by strength he will prevail anyone.
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 Yahweh they will be shattered ([those who] contend against him *Q(K)*) (on him *Q(k)*) in the heavens he will thunder Yahweh he will judge [the] ends of [the] earth so he may give strength to king his and he will exalt [the] horn of anointed his.
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 And he went Elkanah Ramah towards on house his and the lad he was serving Yahweh with [the] presence of Eli the priest.
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 And [the] sons of Eli [were] sons of worthlessness not they knew Yahweh.
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 And [the] custom of the priests with the people every person [who] was sacrificing a sacrifice and he came [the] servant of the priest when boiled the meat and the fork [the] three the prongs [was] in hand his.
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 And he thrust [it] in the pot or in the kettle or in the caldron or in the pot all that it brought up the fork he took the priest for himself thus they did to all Israel who came there at Shiloh.
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Also before they made smoke! the fat and he came - [the] servant of the priest and he said to the man who was sacrificing give! meat to roast to the priest and not he will accept from you meat boiled that except raw.
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 And he said to him the man surely let them make smoke! as the day the fat and take for yourself just as it desires appetite your and he said - (no *Q(K)*) that now you will give [it] and if not I take [it] by force.
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 And it was [the] sin of the young men great very with [the] presence of Yahweh for they treated with contempt the men [the] offering of Yahweh.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 And Samuel [was] serving with [the] presence of Yahweh a lad girded an ephod of linen.
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 And a robe small she made for him mother his and she brought it up to him from days - days towards when went up she with husband her to sacrifice [the] sacrifice of the days.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 And he blessed Eli Elkanah and wife his and he said may he appoint Yahweh for you offspring from the woman this in place of the petition which someone asked to Yahweh and they went to place his.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 For he visited Yahweh Hannah and she conceived and she bore three sons and two daughters and he grew up the lad Samuel with Yahweh.
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 And Eli he was old exceedingly and he heard all that they did! sons his to all Israel and [he heard] this: they were lying with! the women who were serving [the] opening of [the] tent of meeting.
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 And he said to them why? are you doing! according to the things these that I [am] hearing things your wicked from with all the people these.
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 May not [it be] O sons my for [is] not good the report which I [am] hearing [which are] spreading [the] people of Yahweh.
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 If he will sin a person to a person and he will mediate for him God and if to Yahweh he will sin a person who? will he intercede for him and not they listened to [the] voice of father their for he desired Yahweh to put to death them.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 And the lad Samuel [was] going and [was] growing up and he was good both with Yahweh as well as with people.
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 And he came a man of God to Eli and he said to him thus he says Yahweh ¿ really did I reveal myself to [the] house of ancestor your when were they in Egypt to [the] house of Pharaoh.
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 And I chose him from all [the] tribes of Israel for myself to a priest to go up on altar my to make smoke incense to bear an ephod before me and I gave! to [the] house of ancestor your all [the] fire offerings of [the] people of Israel.
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 Why? do you kick at sacrifice my and at offering my which I commanded a dwelling place and you honor sons your more than me by fattening yourselves from [the] choicest of every offering of Israel of people my.
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 Therefore [the] utterance of Yahweh [the] God of Israel certainly I said house your and [the] house of ancestor your they will walk about before me until perpetuity and now [the] utterance of Yahweh far be it to me for [those who] honor me I will honor and [those who] despise me they will be insignificant.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 Here! days [are] coming and I will cut off arm your and [the] arm of [the] house of ancestor your from being an old [man] in house your.
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 And you will look at [the] distress of a dwelling place in all that he will do good to Israel and not he will be an old [man] in house your all the days.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 And a man not I will cut off to you from with altar my to cause to fail eyes your and to cause to grieve self your and all [the] increase of house your they will die men.
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 And this for you [will be] the sign which it will come to [the] two sons your to Hophni and Phinehas on a day one they will die both of them.
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 And I will raise up for myself a priest faithful according to [that] which [is] in heart my and in soul my he will act and I will build for him a house sure (and he will walk about *LAH(b)*) before anointed my all the days.
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 And it will be every [one who] remains in house your he will come to bow down to him for a payment of silver and a round loaf of bread and he will say attach me please to one of the priesthoods to eat a piece of bread.
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >