< 1 Samuel 12 >

1 And he said Samuel to all Israel here! I have listened to voice your to all that you have said to me and I have made king over you a king.
Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 And now here! the king - [is] walking about before you and I I am old and I am gray haired and sons my here they [are] with you and I I have walked about before you since youth my until the day this.
Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
3 Here [am] I testify against me before Yahweh and before anointed his [the] ox of - whom? have I taken and [the] donkey of whom? have I taken and whom? have I oppressed whom? have I crushed and from [the] hand of whom? have I taken a ransom so I may hide eyes my by it so I may restore [it] to you.
Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
4 And they said not you have oppressed us and not you have crushed us and not you have taken from [the] hand of anyone anything.
Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
5 And he said to them [is] a witness Yahweh on you and [is] a witness anointed his the day this that not you have found in hand my anything and someone said [he is] a witness.
Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 And he said Samuel to the people Yahweh who he appointed Moses and Aaron and who he brought up ancestors your from [the] land of Egypt.
Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 And therefore present yourselves so let me enter into judgment with you before Yahweh all [the] righteousness of Yahweh which he did with you and with ancestors your.
Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
8 Just when he went Jacob Egypt and they cried out ancestors your to Yahweh and he sent Yahweh Moses and Aaron and they brought out ancestors your from Egypt and they caused to dwell them in the place this.
“Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 And they forgot Yahweh God their and he sold them in [the] hand of Sisera [the] commander of [the] army of Hazor and in [the] hand of [the] Philistines and in [the] hand of [the] king of Moab and they fought against them.
“Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 And they cried out to Yahweh (and they said *Q(K)*) we have sinned for we have forsaken Yahweh and we have served the Baals and the Ashtaroth and now deliver us from [the] hand of enemies our so we may serve you.
Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 And he sent Yahweh Jerub-Baal and Bedan and Jephthah and Samuel and he delivered you from [the] hand of enemies your from round about and you dwelt security.
Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 And you saw that Nahash [the] king of [the] people of Ammon [was] coming on you and you said to me In-deed a king he will reign over us and Yahweh God your [was] king your.
“Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
13 And now here! the king whom you have chosen whom you asked for and here! he has set Yahweh over you a king.
Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
14 If you will fear Yahweh and you will serve him and you will listen to voice his and not you will rebel against [the] mouth of Yahweh and you will be both you as well as the king who he has become king over you after Yahweh God your.
Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 And if not you will listen to [the] voice of Yahweh and you will rebel against [the] mouth of Yahweh and it will be [the] hand of Yahweh on you and on ancestors your.
Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 Also now stand and see the thing great this which Yahweh [is] about to do to eyes your.
“Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 ¿ Not [is] [the] harvest of wheat this day I will call out to Yahweh so he may give thunder claps and rain and know and see that evil your [is] great which you have done in [the] eyes of Yahweh by asking for yourselves a king.
Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
18 And he called out Samuel to Yahweh and he gave Yahweh thunder claps and rain on the day that and it feared all the people exceedingly Yahweh and Samuel.
Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
19 And they said all the people to Samuel pray for servants your to Yahweh God your and may not we die for we have added to all sins our an evil thing by asking for ourselves a king.
Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 And he said Samuel to the people may not you be afraid you you have done all the evil this nevertheless may not you turn aside from after Yahweh and you will serve Yahweh with all heart your.
Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
21 And not you must turn aside for - after emptiness which not they will benefit and not they will rescue for [are] emptiness they.
Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 For not he will abandon Yahweh people his for sake of name his great for he was determined Yahweh to make you for himself into a people.
Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
23 Also I far be it to me from sinning to Yahweh from ceasing to pray for you and I will teach you [the] way of the good and the upright.
Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
24 Only - fear Yahweh and you will serve him in faithfulness with all heart your for consider this: he has done great things with you.
Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 And if still you will do evil both you as well as king your you will be swept away.
Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”

< 1 Samuel 12 >