< 1 Kings 6 >

1 And it was in eighty year and four hundred year of [the] coming out of [the] people of Israel from [the] land of Egypt in the year fourth in [the] month of Ziv that [was] the month second of [the] reigning of Solomon over Israel and he built the house for Yahweh.
Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Solomoni katika Israeli, katika mwezi wa Zivu, ambao ndio mwezi wa pili, alianza kujenga Hekalu la Bwana.
2 And the house which he built the king Solomon for Yahweh [was] sixty cubit[s] length its and [was] twenty breadth its and [was] thirty cubit[s] height its.
Hekalu hilo Mfalme Solomoni alilojenga kwa ajili ya Bwana lilikuwa na urefu wa dhiraa sitini, upana wa dhiraa ishirini na kimo cha dhiraa thelathini kwenda juu.
3 And the porch on [the] face of [the] temple of the house [was] twenty cubit[s] length its on [the] face of [the] breadth of the house [was] ten by the cubit breadth its on [the] face of the house.
Baraza ya mbele ya Hekalu ilienea dhiraa ishirini kulingana na upana wa Hekalu na kujitokeza dhiraa kumi mbele ya Hekalu.
4 And he made for the house windows of frames shut.
Akatengeneza madirisha membamba yenye vidirisha vidogo vya juu katika Hekalu.
5 And he built on [the] wall of the house (an extension *Q(K)*) all around [the] walls of the house around the temple and the innermost room and he made side-chambers all around.
Akafanyiza vyumba vya pembeni kulizunguka Hekalu lote vikishikamana na kuta za Hekalu na za Patakatifu pa Patakatifu.
6 (The extension *Q(K)*) lower [was] five by the cubit breadth its and the middle [extension] [was] six by the cubit breadth its and third [extension] [was] seven by the cubit breadth its for ledges he made for the house around [the] outside towards to not to have hold in [the] walls of the house.
Ghorofa ya chini kabisa ilikuwa na upana wa dhiraa tano, ya kati ilikuwa dhiraa sita na ya tatu ilikuwa dhiraa saba. Kuzunguka ukuta wa nje wa Hekalu akapunguza ukuta pande zote ili boriti zisishikane kwenye kuta za Hekalu.
7 And the house when was built it stone perfect quarry it was built and hammers and axe any article of iron not it was heard in the house when was built it.
Katika kujenga Hekalu, yalitumika tu mawe yaliyochongwa huko machimboni, wala hakuna nyundo, patasi au chombo kingine chochote cha chuma kilichosikika sauti yake katika eneo la ujenzi wa Hekalu wakati lilipokuwa likijengwa.
8 [the] entrance of The side-chamber middle [was] to [the] side of the house south and by stairs people went up to the middle and from the middle to the thirty.
Ingilio la ghorofa ya chini kabisa lilikuwa upande wa kusini wa Hekalu, ngazi ilielekea ghorofa ya kati na kutokea hapo ilielekea hadi ghorofa ya tatu.
9 And he built the house and he finished it and he covered the house beams and planks with cedar.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha, akiliweka paa za boriti na mbao za mierezi.
10 And he built (the extension *Q(K)*) on all the house [was] five cubits height its and he covered the house with wood of cedar.
Mfalme Solomoni akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka Hekalu lote. Kimo cha kila kimoja kilikuwa dhiraa tano. Navyo vilikuwa vimeunganishwa na Hekalu kwa boriti za mierezi.
11 And it came [the] word of Yahweh to Solomon saying.
Neno la Bwana likamjia Solomoni kusema:
12 The house this which you [are] building if you will walk in statutes my and judgments my you will observe and you will keep all commandments my to walk in them and I will establish word my with you which I spoke to David father your.
“Kwa habari ya Hekalu hili unalojenga, kama ukifuata amri zangu, ukatunza masharti yangu na kushika maagizo yangu yote na kuyatii, kwa kupitia wewe nitatimiza ahadi niliyomwahidi Daudi baba yako.
13 And I will dwell in among [the] people of Israel and not I will abandon people my Israel.
Nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli, nami sitawaacha watu wangu Israeli.”
14 And he built Solomon the house and he finished it.
Basi Solomoni akajenga Hekalu na kulikamilisha.
15 And he built [the] walls of the house from inside with boards of cedar from [the] floor of the house to [the] walls of the ceiling he overlaid wood from inside and he overlaid [the] floor of the house with boards of cypresses.
Akazifunika kuta zake za ndani kwa mbao za mierezi, akizipigilia ukutani kuanzia sakafuni mwa Hekalu hadi kwenye dari na kufunika sakafu ya Hekalu kwa mbao za misunobari.
16 And he built twenty cubit[s] (from [the] innermost parts of *Q(k)*) the house with boards of cedar from the floor to the walls and he built for it from inside to an innermost room to [the] holy place of the holy places.
Akagawa dhiraa ishirini sehemu ya nyuma ya Hekalu kwa mbao za mierezi kuanzia kwenye sakafu hadi darini ili kufanya sehemu takatifu ya ndani, yaani Patakatifu pa Patakatifu.
17 And forty by the cubit it was the house that [is] the temple before me.
Ukumbi mkubwa uliokuwa mbele ya chumba hiki ndio ulikuwa na urefu wa dhiraa arobaini.
18 And cedar [was] to the house within carving of gourds and spread out [things] of flowers everything [was] cedar not stone [was] visible.
Hekalu ndani ilikuwa ya mierezi iliyonakshiwa mifano ya maboga na maua yaliyochanua. Kila kitu kilikuwa cha mwerezi, hakuna jiwe ambalo lilionekana.
19 And an innermost room in [the] middle of the house from within he prepared to put there [the] ark of [the] covenant of Yahweh.
Ndani ya Hekalu akatengeneza sehemu takatifu ya ndani, kwa ajili ya kuweka Sanduku la Agano la Bwana.
20 And before the innermost room [was] twenty cubit[s] length and [was] twenty cubit[s] breadth and [was] twenty cubit[s] height its and he overlaid it gold gold plate and he overlaid an altar cedar.
Sehemu takatifu ya ndani ilikuwa na upana, urefu na kimo cha dhiraa ishirini ndani kwa ndani. Akaifunika ndani kwa dhahabu safi, pia akaifunika madhabahu ya mierezi vivyo hivyo.
21 And he overlaid Solomon the house from within gold gold plate and he made pass (with chains of *Q(K)*) gold before the innermost room and he overlaid it gold.
Solomoni akaifunika sehemu ya ndani ya Hekalu kwa dhahabu safi, naye akaitandaza mikufu ya dhahabu kutoka upande moja hadi ule mwingine mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, ambako palifunikwa kwa dhahabu.
22 And all the house he overlaid gold until was finished all the house and all the altar which [belonged] to the innermost room he overlaid gold.
Basi akafunika sehemu yote ya ndani kwa dhahabu. Pia akafunika madhabahu yale yaliyokuwa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu kwa dhahabu.
23 And he made in the innermost room two cherubim wood of olive [was] ten cubits height its.
Katika Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza makerubi wawili kwa mzeituni, kila moja likiwa na dhiraa kumi kwenda juu.
24 And [was] five cubits [the] wing of the cherub one and [was] five cubits [the] wing of the cherub second [was] ten cubits from [the] ends of wings its and to [the] ends of wings its.
Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na bawa jingine dhiraa tano, hivyo urefu kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa jingine ulikuwa dhiraa kumi.
25 And [was] ten by the cubit the cherub second a measurement one and a shape one [belonged] to [the] two the cherubim.
Kerubi wa pili alikuwa na urefu wa dhiraa kumi pia, hivyo makerubi hao wawili walifanana kwa vipimo na kwa umbo.
26 [the] height of The cherub one [was] ten by the cubit and thus the cherub second.
Kimo cha kila kerubi kilikuwa dhiraa kumi.
27 And he put the cherubim in [the] middle of - the house inner and they spread out [the] wings of the cherubim and it touched [the] wing of the one [cherub] the wall and [the] wing of the cherub second [was] touching the wall second and wings their to [the] middle of the house [were] touching wing to wing.
Aliwaweka makerubi hao ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pa Hekalu, mabawa yake yakiwa yamekunjuliwa. Bawa la kerubi mmoja liligusa ukuta mmoja, wakati bawa la yule mwingine liligusa ukuta mwingine, nayo mabawa yao mengine yaligusana katikati ya chumba.
28 And he overlaid the cherubim gold.
Akafunika wale makerubi kwa dhahabu.
29 And all [the] walls of the house round about - he carved engravings of carvings of cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers from to faces and to the outer.
Juu ya kuta zote zilizozunguka Hekalu, za vyumba vya ndani na vya nje, zilipambwa kwa nakshi zilizokatwa za makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua.
30 And [the] floor of the house he overlaid gold to within and to the outer.
Pia alifunika sakafu zote za vyumba vya ndani na vya nje vya Hekalu kwa dhahabu.
31 And [the] entrance of the innermost room he made doors of wood of olive the pillar doorposts of fifth.
Kwa ingilio la Patakatifu pa Patakatifu akatengeneza milango ya mbao za mzeituni, zikiwa na miimo na vizingiti vyenye umbo la pembe tano.
32 And two doors of wood of olive and he carved on them carvings of cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers and he overlaid [them] gold and he hammered out on the cherubim and on the palm trees the gold.
Juu ya milango miwili ya mbao za mzeituni alinakshi makerubi, miti ya mitende pamoja na maua yaliyochanua na kufunika makerubi na miti ya mitende kwa dhahabu iliyofuliwa.
33 And thus he made for [the] entrance of the temple doorposts of wood of olive from with a fourth.
Kwa njia iyo hiyo akatengeneza miimo yenye pande nne ya miti ya mizeituni, kwa ajili ya ingilio la ukumbi mkubwa.
34 And two doors of wood of cypresses two sides the door one [were] revolving and two curtains the door second [were] revolving.
Kulikuwa na milango miwili iliyoweza kukunjuka iliyotengenezwa kwa mbao za msunobari na kila mmoja ulikuwa na bawaba ambazo zingeuwezesha kujikunja kila kipande juu ya kingine.
35 And he carved cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers and he overlaid gold made smooth on the carved [work].
Akanakshi makerubi, miti ya mitende na maua yaliyochanua juu yake na kufunika kwa dhahabu iliyonyooshwa vizuri juu ya michoro.
36 And he built the court inner three rows of hewn [stone] and a row of beams of cedar.
Tena akajenga ua wa ndani safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa.
37 In the year fourth it was founded [the] house of Yahweh in [the] month of Ziv.
Msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa katika mwaka wa nne, katika mwezi wa Zivu, ndio mwezi wa tano.
38 And in the year one [plus] ten in [the] month of Bul that [was] the month eighth it was complete the house to all parts its and to all (plans its *Q(K)*) and he built it seven years.
Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa Buli, ndio mwezi wa nane, Hekalu lilikamilika katika hatua zake zote kwa kufuatana na maelekezo yake Solomoni. Alilijenga kwa miaka saba.

< 1 Kings 6 >