< 1 Kings 11 >

1 And the king Solomon he loved women foreign many and [the] daughter of Pharaoh Moabite [women] Ammonite [women] Edomite [women] Sidonian [women] Hittite [women].
Hata hivyo, Mfalme Solomoni akawapenda wanawake wengi wa kigeni zaidi, mbali na binti Farao: wanawake wa Wamoabu, Waamoni, Waedomu, Wasidoni na Wahiti.
2 From the nations which he had said Yahweh to [the] people of Israel not you must go among them and they not they will go among you truly they will turn aside heart your after gods their to them he cleaved Solomon to love [them].
Walitoka katika mataifa ambayo Bwana aliwaambia Waisraeli, “Msije mkaoana nao, kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu mgeukie miungu yao.” Hata hivyo, Solomoni akakaza kuwapenda.
3 And it belonged to him wives noble ladies seven hundred and concubines three hundred and they turned aside wives his heart his.
Alikuwa na wake 700 mabinti wa uzao wa kifalme, na masuria 300, nao wake zake wakampotosha.
4 And it was to [the] time of [the] old age of Solomon wives his they turned aside heart his after gods other and not it was heart his complete with Yahweh God his like [the] heart of David father his.
Kadiri Solomoni alivyozidi kuzeeka, wake zake wakaugeuza moyo wake kuelekea miungu mingine, na moyo wake haukujitolea kikamilifu kwa Bwana Mungu wake, kama ulivyokuwa moyo wa Daudi baba yake.
5 And he walked Solomon after Astarte [the] god of [the] Sidonians and after Milcom [the] detestable thing of [the] Ammonites.
Solomoni akafuata Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, na Moleki mungu aliyekuwa chukizo la Waamoni.
6 And he did Solomon the evil in [the] eyes of Yahweh and not he filled after Yahweh like David father his.
Kwa hiyo Solomoni akafanya uovu machoni pa Bwana; hakumfuata Bwana kikamilifu kama alivyofanya Daudi baba yake.
7 Then he built Solomon a high place for Chemosh [the] detestable thing of Moab on the mountain which [is] on [the] face of Jerusalem and for Molech [the] detestable thing of [the] people of Ammon.
Kwenye kilima mashariki mwa Yerusalemu, Solomoni akajenga mahali pa juu kwa ajili ya Kemoshi chukizo la Wamoabu, na kwa Moleki mungu chukizo la Waamoni.
8 And thus he did for all wives his foreign [who] made smoke and [who] sacrificed to gods their.
Akafanya hivyo kwa wake zake wote wa kigeni, ambao walifukiza uvumba na kutoa dhabihu kwa miungu yao.
9 And he was angry Yahweh with Solomon for it had turned aside heart his from with Yahweh [the] God of Israel who had appeared to him two times.
Bwana akamkasirikia Solomoni kwa sababu moyo wake uligeuka mbali na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa amemtokea mara mbili.
10 And he had commanded to him on the matter this to not to walk after gods other and not he observed [that] which he had commanded Yahweh.
Ingawa alikuwa amemkataza Solomoni kufuata miungu mingine, Solomoni hakutii amri ya Bwana.
11 And he said Yahweh to Solomon because that it has been this with you and not you have observed covenant my and statutes my which I commanded to you certainly I will tear away the kingdom from with you and I will give it to servant your.
Kwa hiyo Bwana akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa hii ndiyo hali yako na hukushika Agano langu na sheria zangu nilizokuamuru, hakika nitaurarua ufalme kutoka kwako na kumpa mmoja wa walio chini yako.
12 Only in days your not I will do it for [the] sake of David father your from [the] hand of son your I will tear away it.
Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi baba yako, sitafanya jambo hili wakati wa uhai wako. Nitaurarua kutoka mikononi mwa mwanao.
13 Only all the kingdom not I will tear away a tribe one I will give to son your for [the] sake of David servant my and for [the] sake of Jerusalem which I have chosen.
Lakini pia sitaurarua ufalme wote kutoka kwake, bali nitampa kabila moja kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu na kwa ajili ya Yerusalemu, ambao nimeuchagua.”
14 And he raised up Yahweh an adversary to Solomon Hadad the Edomite [was] one of [the] offspring the king he in Edom.
Kisha Bwana akamwinua adui dhidi ya Solomoni, Hadadi, Mwedomu, kutoka ukoo wa ufalme wa Edomu.
15 And it was when was David Edom when went up Joab [the] commander of the army to bury the [ones] slain and he struck down every male in Edom.
Huko nyuma wakati Daudi alipokuwa akipigana na Edomu, Yoabu jemadari wa jeshi, aliyekuwa amekwenda kuzika waliouawa, alikuwa amewaua wanaume wote waliokuwako Edomu.
16 For six months he remained there Joab and all Israel until he had cut off every male in Edom.
Yoabu na Waisraeli wote walikaa huko kwa miezi sita, mpaka walipomaliza kuwaangamiza wanaume wote huko Edomu.
17 And he fled Hadad he and people Edomite some of [the] servants of father his with him to go Egypt and Hadad [was] a youth young.
Lakini Hadadi, akiwa bado mvulana mdogo, alikimbilia Misri akiwa na baadhi ya maafisa wa Kiedomu waliokuwa wakimhudumia baba yake.
18 And they arose from Midian and they went Paran and they took men with them from Paran and they went Egypt to Pharaoh [the] king of Egypt and he gave to him a house and food he assigned to him and land he gave to him.
Wakaondoka Midiani wakaenda Parani. Basi wakichukua pamoja nao wanaume kutoka Parani, wakaenda Misri, kwa Farao mfalme wa Misri, ambaye alimpa Hadadi nyumba, ardhi na akampatia chakula.
19 And he found Hadad favor in [the] eyes of Pharaoh exceedingly and he gave to him a wife [the] sister of own wife his [the] sister of Tahpenes the queen.
Farao akapendezwa sana na Hadadi hata akampa ndugu wa mkewe mwenyewe, Malkia Tapenesi, ili aolewe na Hadadi.
20 And she bore to him [the] sister of Tahpenes Genubath son his and she weaned him Tahpenes in [the] midst of [the] household of Pharaoh and he was Genubath [the] house of Pharaoh in among [the] sons of Pharaoh.
Huyo ndugu wa Tapenesi akamzalia mwana aliyeitwa Genubathi, ambaye alilelewa na Tapenesi katika jumba la kifalme. Huko Genubathi aliishi pamoja na watoto wa Farao mwenyewe.
21 And Hadad he heard in Egypt that he had lain down David with ancestors his and that he had died Joab [the] commander of the army and he said Hadad to Pharaoh let go me so I may go to own land my.
Alipokuwa huko Misri, Hadadi alisikia kwamba Daudi amepumzika na baba zake na ya kwamba pia Yoabu aliyekuwa jemadari wa jeshi amekufa. Ndipo Hadadi akamwambia Farao, “Niruhusu niende ili niweze kurudi katika nchi yangu.”
22 And he said to him Pharaoh that what? [are] you lacking with me and here you [are] seeking to go to own land your and he said - In-deed really you will let go me.
Farao akauliza, “Umekosa nini hapa, kwamba unataka kurudi katika nchi yako?” Hadadi akajibu, “Hakuna, lakini niruhusu niende!”
23 And he raised up God to him an adversary Rezon [the] son of Eliada who he had fled from with Hadadezer [the] king of Zobah master his.
Mungu akamwinua adui mwingine dhidi ya Solomoni, Rezoni mwana wa Eliada, ambaye alikuwa amemkimbia bwana wake Hadadezeri, mfalme wa Soba.
24 And he gathered with him men and he was [the] leader of a marauding band when killed David them and they went Damascus and they dwelt in it and they reigned in Damascus.
Akawakusanya watu, naye akawa kiongozi wa kundi la waasi, wakati Daudi alipoangamiza majeshi ya Soba; waasi walikwenda Dameski, mahali walipokaa na kumiliki.
25 And he was an adversary of Israel all [the] days of Solomon and harm which Hadad and he loathed Israel and he reigned over Aram.
Rezoni alikuwa adui wa Israeli kwa muda wote alioishi Solomoni, ukiongezea matatizo yaliyosababishwa na Hadadi. Kwa hiyo Rezoni akatawala katika Aramu na alikuwa mkatili kwa Israeli.
26 And Jeroboam [the] son of Nebat an Ephrathite from Zeredah and [the] name of mother his [was] Zeruah a woman a widow a servant of Solomon and he raised a hand on the king.
Pia, Yeroboamu mwana wa Nebati aliasi dhidi ya mfalme. Alikuwa mmoja wa maafisa wa Solomoni, Mwefraimu kutoka Sereda, ambaye mama yake alikuwa mjane aliyeitwa Serua.
27 And this [is] the reason why he raised a hand on the king Solomon he built the Millo he closed up [the] breach of [the] city of David father his.
Haya ndiyo maelezo ya jinsi alivyomwasi mfalme: Solomoni alikuwa amejenga Milo naye akawa ameziba mwanya katika ukuta wa mji wa Daudi baba yake.
28 And the man Jeroboam [was] a mighty [man] of strength and he saw Solomon the young man that [was] doing work he and he appointed him to all [the] forced labor of [the] house of Joseph.
Basi Yeroboamu alikuwa mtu shujaa na hodari, naye Solomoni alipoona jinsi kijana alivyofanya kazi yake, akamweka kuwa kiongozi wa kazi yote ya mikono ya nyumba ya Yosefu.
29 And it was at the time that and Jeroboam he had gone out from Jerusalem and he found him Ahijah Shilonite the prophet on the way and he [was] covering himself with a cloak new and [the] two of them to alone them [were] in the open country.
Karibu na wakati ule Yeroboamu alikuwa anatoka nje ya Yerusalemu, Ahiya nabii Mshiloni akakutana naye njiani, akiwa amevaa joho jipya. Hawa wawili walikuwa peke yao mashambani,
30 And he seized Ahijah the cloak new which [was] on him and he tore it two [plus] ten pieces.
naye Ahiya akachukua joho jipya alilokuwa amevaa akalirarua vipande kumi na viwili.
31 And he said to Jeroboam take for yourself ten pieces for thus he says Yahweh [the] God of Israel here I [am] about to tear the kingdom from [the] hand of Solomon and I will give to you ten the tribes.
Kisha akamwambia Yeroboamu, “Chukua vipande kumi kwa ajili yako, kwa kuwa hivi ndivyo Bwana, Mungu wa Israeli asemavyo: ‘Tazama, ninakwenda kuuchana ufalme kutoka mikononi mwa Solomoni na kukupa wewe makabila kumi.
32 And the tribe one it will belong to him for [the] sake of - servant my David and for [the] sake of Jerusalem the city which I have chosen it from all [the] tribes of Israel.
Lakini kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi na mji wa Yerusalemu, ambao nimeuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli, atakuwa na kabila moja.
33 Because - that they have forsaken me and they have bowed down to Astarte [the] god of [the] Sidonians to Chemosh [the] god of Moab and to Milcom [the] god of [the] people of Ammon and not they have walked in ways my by doing the right in view my and statutes my and judgments my like David father his.
Nitafanya hivi kwa sababu wameniacha mimi na kuabudu Ashtorethi mungu mke wa Wasidoni, Kemoshi mungu wa Wamoabu, na Moleki mungu wa Waamoni, nao hawakwenda katika njia zangu ili kufanya yaliyo sawa machoni pangu, wala kushika amri na sheria zangu kama Daudi, babaye Solomoni, alivyofanya.
34 And not I will take all the kingdom from hand his for - ruler I will make him all [the] days of life his for [the] sake of David servant my whom I chose him who he observed commandments my and statutes my.
“‘Lakini sitauondoa ufalme wote kutoka mikononi mwa Solomoni, nimemfanya mtawala siku zote za maisha yake kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, niliyemchagua na ambaye aliyatunza maagizo na amri zangu.
35 And I will take the kingship from [the] hand of son his and I will give it to you [the] ten the tribes.
Nitauondoa ufalme kutoka mikononi mwa mwanawe na kukupa wewe makabila kumi.
36 And to son his I will give a tribe one so as to belong a lamp to David servant my all the days - before me in Jerusalem the city which I have chosen for myself to put name my there.
Nitampa mwanawe kabila moja ili kwamba Daudi mtumishi wangu awe na taa mbele zangu daima katika Yerusalemu, mji ambao nimeuchagua kuweka Jina langu.
37 And you I will take and you will reign over all that it will desire self your and you will be king over Israel.
Hata hivyo, kukuhusu wewe Yeroboamu, nitakutwaa, nawe utatawala juu ya yote yale moyo wako unayotamani, utakuwa mfalme juu ya Israeli.
38 And it will be if you will listen to all that I will command you and you will walk in ways my and you will do the right in view my by observing statutes my and commandments my just as he did David servant my and I will be with you and I will build for you a house enduring just as I built for David and I will give to you Israel.
Ikiwa utafanya kila nitakalokuamuru, kuenenda katika njia zangu na kufanya yaliyo sawa mbele za macho yangu kwa kuzishika amri zangu na maagizo yangu kama alivyofanya Daudi mtumishi wangu, nitakuwa pamoja nawe. Nitakujengea ufalme utakaodumu kama ule niliomjengea Daudi, nami nitakupa Israeli.
39 So I may afflicted [the] offspring of David on account of this nevertheless not all the days.
Nitawatesa wazao wa Daudi kwa ajili ya hili, lakini siyo milele.’”
40 And he sought Solomon to put to death Jeroboam and he arose Jeroboam and he fled Egypt to Shishak [the] king of Egypt and he was in Egypt until [the] death of Solomon.
Solomoni akajaribu kumuua Yeroboamu, lakini Yeroboamu akakimbilia Misri, kwa Mfalme Shishaki, naye akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.
41 And [the] rest of [the] matters of Solomon and all that he did and wisdom his ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of Solomon.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, yote aliyoyafanya na hekima aliyoionyesha, je hayakuandikwa yote katika kitabu cha matendo cha Solomoni?
42 And the days which he reigned Solomon in Jerusalem over all Israel [were] forty year[s].
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
43 And he lay down Solomon with ancestors his and he was buried in [the] city of David father his and he became king Rehoboam son his in place of him.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 1 Kings 11 >