< 1 Corinthians 8 >
1 Concerning now the idol-sacrifices, we know indeed all knowledge we have. Knowledge puffs up, but love builds up.
Yahusu sasa vyakula vilivyotambikiwa sanamu: Tunajua kwamba sisi sote tuna ujuzi, lakini ujuzi huo huwafanya watu wawe na majivuno; lakini mapendo hujenga.
2 If (now *k*) anyone thinks (to have known *N(k)O*) anything, (not yet *N(k)O*) (no [thing] *k*) (he knew *N(k)O*) even as it is necessary to know;
Anayefikiri kwamba anajua kitu, kwa kweli hajui chochote kama inavyompasa.
3 If however anyone loves God, he has known by Him.
Lakini anayempenda Mungu huyo anajulikana naye.
4 Concerning the eating therefore of the idol-sacrifices we know that no [thing] an idol [is] in [the] world and that [there is] no God (other *k*) only except one.
Kwa hiyo, kuhusu vyakula vilivyotambikiwa sanamu, twajua kwamba sanamu si kitu duniani; twajua kwamba Mungu ni mmoja tu.
5 Even truly if indeed if indeed there are [those] named gods whether in heaven or on (*k*) earth, as there are gods many and lords many;
Hata kama viko vitu viitwavyo miungu duniani au mbinguni, na hata kama wako miungu na mabwana wengi,
6 yet to us [there is] one God the Father of whom [are] the [things] all and we ourselves for Him, and one Lord Jesus Christ through whom [are] the [things] all and we ourselves through Him.
hata hivyo, kwetu sisi yuko Mungu mmoja tu: Baba, Muumba wa vyote, ambaye kwa ajili yake sisi tuko. Pia yuko Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, na sisi twaishi kwa njia yake.
7 But not in all [is] this knowledge; Some now (by custom *N(K)O*) until now of the idol as of an idol-sacrifice eat, and the conscience of them weak being it is defiled.
Lakini, si kila mtu anao ujuzi huu. Maana wako watu wengine waliokwisha zoea sanamu, watu ambao mpaka hivi sasa wanapokula vyakula huviona bado kama vyakula vilivyotambikiwa sanamu. Na kwa vile dhamiri zao ni dhaifu, hutiwa unajisi.
8 Food however us not (will commend *N(k)O*) to God; neither (for *ko*) if not we shall eat [still] do we come short [then] nor if we shall eat (have we an advantage. *NK(o)*)
Lakini chakula hakiwezi kutupeleka karibu zaidi na Mungu. Tukiacha kukila hatupungukiwi kitu, tukikila hatuongezewi kitu.
9 do be careful however lest perhaps the right of you this an occasion of stumbling may become to those (weak. *N(k)O*)
Lakini, jihadharini: huu uhuru wenu usiwafanye walio na imani dhaifu waanguke katika dhambi.
10 If for anyone shall see you who is having knowledge in an idol’s temple eating, surely the conscience of him weak being he will be encouraged the idol-sacrifices to eat?
Maana, mtu ambaye dhamiri yake ni dhaifu, akikuona wewe mwenye ujuzi unakula vyakula hivyo ndani ya hekalu la sanamu, je, hatatiwa moyo wa kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu?
11 (Is destroyed *N(K)O*) (for *N(k)O*) the [one] who is being weak (through *N(k)O*) your knowledge, (the *no*) brother for whom Christ died.
Hivyo, huyo ndugu yako dhaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea kwa sababu ya ujuzi wako.
12 Thus then sinning against the brothers and wounding their conscience being weak, against Christ you sin.
Kama mkiwakosesha ndugu zenu jinsi hiyo na kuzijeruhi dhamiri zao dhaifu, mtakuwa mmemkosea Kristo.
13 Therefore if food snares the brother of mine, certainly not shall I eat meat to the age so that not the brother of mine I may snare. (aiōn )
Kwa hiyo, ikiwa chakula husababisha kuanguka kwa ndugu yangu, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi. (aiōn )