< 1 Chronicles 22 >

1 And he said David this it [is] [the] house Yahweh God and this [is the] altar for burnt offering for Israel.
Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
2 And he said David to gather the sojourners who [were] in [the] land of Israel and he appointed stone cutters to cut stones of hewn [stone] to build [the] house of God.
Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
3 And iron - to abundance for the nails for [the] doors of the gates and for the clamps he prepared David and bronze to abundance there not [was] weight.
Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
4 And wood of cedar to there not [was] number for they had brought the Sidonians and the Tyrians wood of cedar to abundance to David.
Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
5 And he said David Solomon son my [is] a youth and weak and the house to build for Yahweh [is] to make great - upwards for a name and for honor to all the lands I will prepare please for it and he prepared David to abundance before death his.
Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
6 And he summoned Solomon son his and he commanded him to build a house for Yahweh [the] God of Israel.
Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
7 And he said David to Solomon (O son my *Q(K)*) I it was with heart my to build a house for [the] name of Yahweh God my.
Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
8 And it came to me [the] word of Yahweh saying blood to abundance you have shed and wars great you have made not you will build a house for name my for blood much you have shed [the] ground towards before me.
Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
9 Here! a son [is] about to be born to you he he will be a man of rest and I will give rest to him from all enemies his from round about for Solomon it will be name his and peace and quietness I will give to Israel in days his.
Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
10 He he will build a house for name my and he he will become of me a son and I of him a father and I will establish [the] throne of kingdom his over Israel until perpetuity.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
11 Now O son my may he be Yahweh with you and you will be successful and you will build [the] house of Yahweh God your just as he spoke on you.
“Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
12 Only may he give to you Yahweh insight and understanding and he will appoint you over Israel and to keep [the] law of Yahweh God your.
Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
13 Then you will be successful if you will take care to observe the statutes and the judgments which he commanded Yahweh Moses on Israel be strong and be courageous may not you be afraid and may not you be dismayed.
Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
14 And here! in affliction my I have prepared for [the] house of Yahweh gold talents one hundred thousand and silver one thousand thousand talents and [belongs] to the bronze and to the iron not weight for to abundance it is and wood and stone I have prepared and to them you will add.
“Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
15 And [are] with you to abundance doers of work stone cutters and craftsmen of stone and wood and every skillful [person] in every work.
Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
16 Of gold of silver and of bronze and of iron there not [is] number arise and act so may he be Yahweh with you.
wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
17 And he commanded David to all [the] officials of Israel to help Solomon son his.
Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
18 ¿ Not [is] Yahweh God your with you and has he given rest? to you from round about for - he has given in hand my [the] inhabitants of the land and it has been subdued the land before Yahweh and before people his.
Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
19 Now set heart your and being your to seek Yahweh God your and arise and build [the] sanctuary of Yahweh God to bring [the] ark of [the] covenant of Yahweh and [the] articles of holiness of God to the house that will be built for [the] name of Yahweh.
Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”

< 1 Chronicles 22 >