< 1 Chronicles 19 >

1 And it was after thus and he died Nahash [the] king of [the] people of Ammon and he reigned son his in place of him.
Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
2 And he said David I will do loyalty - with Hanun [the] son of Nahash for he did father his with me loyalty and he sent David messengers to comfort him on father his and they came [the] servants of David into [the] land of [the] people of Ammon to Hanun to comfort him.
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
3 And they said [the] officials of [the] people of Ammon to Hanun ¿ [is] honoring David father your in view your for he has sent to you comforters ¿ not in order to explore and to overthrow and to spy out the land have they come servants his to you.
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
4 And he took Hanun [the] servants of David and he shaved them and he cut off robes their in the middle to the buttock[s] and he sent away them.
Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 And people went and they told to David on the men and he sent to meet them for they were the men humiliated exceedingly and he said the king remain at Jericho until that it will grow back beard your and you will return.
Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
6 And they saw [the] people of Ammon that they had made themselves odious with David and he sent Hanun and [the] people of Ammon one thousand talent[s] of silver to hire for themselves from Aram Naharaim and from Aram Maacah and from Zobah chariotry and horsemen.
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
7 And they hired for themselves two and thirty thousand chariot[s] and [the] king of Maacah and people his and they came and they encamped before Medeba and [the] people of Ammon they gathered from cities their and they came for battle.
Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
8 And he heard David and he sent Joab and all [the] army the warriors.
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
9 And they went out [the] people of Ammon and they deployed battle [the] entrance of the city and the kings who they had come to alone them [were] in the open country.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
10 And he saw Joab that it was [the] face of the battle against him face and back and he chose from every chosen [man] in Israel and he deployed to meet Aram.
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
11 And [the] rest of the people he put in [the] hand of Abishai brother his and they deployed to meet [the] people of Ammon.
Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
12 And he said if it will be [too] strong for me Aram and you will become for me deliverance. And if [the] people of Ammon they will be [too] strong for you and I will deliver you.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
13 Be strong so let us show ourselves strong for people our and for [the] cities of God our and Yahweh the good in view his he will do.
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
14 And he drew near Joab and the people which [was] with him before Aram for battle and they fled from before him.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
15 And [the] people of Ammon they saw that it had fled Aram and they fled also they from before Abishai brother his and they went the city towards and he went Joab Jerusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
16 And it saw Aram that they had been defeated before Israel and they sent messengers and they brought out Aram which [was] from [the] other side of the river and Shophach [the] commander of [the] army of Hadadezer [was] before them.
Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
17 And it was told to David and he gathered all Israel and he passed over the Jordan and he came to them and he deployed against them and he deployed David to meet Aram battle and they fought with him.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
18 And it fled Aram from to before Israel and he killed David of Aram seven thousand charioteer[s] and forty thousand man on foot and Shophach [the] commander of the army he killed.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
19 And they saw [the] servants of Hadadezer that they had been defeated before Israel and they made peace with David and they served him and not it was willing Aram to deliver [the] people of Ammon again.
Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.

< 1 Chronicles 19 >