< Zechariah 12 >
1 The oracle of the word of Yahweh, on Israel, —Declareth Yahweh—Stretching out the heavens, and founding the earth, and fashioning the spirit of man within him:
Hili ni neno la Bwana kuhusu Israeli. Bwana, yeye azitandaye mbingu, awekaye misingi ya dunia na aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake, asema:
2 Lo! I am making Jerusalem a bowl of reeling to all the peoples, round about, —Moreover also, on Judah, shall it be in the siege against Jerusalem;
“Nitakwenda kufanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumbisha mataifa yote yanayoizunguka. Yuda utazingirwa kwa vita na Yerusalemu pia.
3 And it shall come to pass, in that day, that I will make Jerusalem a lifting-stone, to all the peoples, all who seek to lift her, shall, cut themselves in pieces, —though all the nations of the earth, gather themselves together against her.
Katika siku hiyo, wakati mataifa yote ya dunia yatakapokusanyika dhidi yake, nitaufanya Yerusalemu kuwa jabali lisilosogezwa kwa mataifa yote. Wote watakaojaribu kulisogeza watajiumiza wenyewe.
4 In that day, Declareth Yahweh, I will smite every horse with terror, and his rider with madness, —and, over the house of Judah, will I keep opening mine eyes, and, every horse of the peoples, will I smite with blindness.
Katika siku hiyo nitampiga kila farasi kwa hofu ya ghafula, naye ampandaye nitampiga kwa uwazimu,” asema Bwana. “Nitalielekeza jicho langu la ulinzi juu ya nyumba ya Yuda, nami nitawapofusha farasi wote wa mataifa.
5 Then will the chiefs of Judah say in their hearts, —A strength unto me, [would be] the inhabitants of Jerusalem, in Yahweh of hosts, their God.
Kisha viongozi wa Yuda watasema mioyoni mwao, ‘Watu wa Yerusalemu wana nguvu kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu wao.’
6 In that day, will I make the chiefs of Judah like a pan of fire among sticks, and like a torch of fire in a sheaf, so shall they devour, on the right hand and on the left, all the peoples round about; so shall Jerusalem yet, be inhabited, in her own place, as Jerusalem.
“Katika siku hiyo nitawafanya viongozi wa Yuda kuwa kama kigae cha moto ndani ya lundo la kuni, kama mwenge uwakao kati ya miganda. Watateketeza kulia na kushoto mataifa yote yanayowazunguka, lakini Yerusalemu utabaki salama mahali pake.
7 But Yahweh will save the tents of Judah first, —lest the honour of the house of David, and the honour of the inhabitant of Jerusalem, should be magnified over Judah.
“Bwana atayaokoa makao ya Yuda kwanza, ili heshima ya nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu isiwe kubwa zaidi kuliko ile ya Yuda.
8 In that day, will Yahweh, throw a covering, around the inhabitant of Jerusalem, so shall the tottering among them, in that day, become like David, —and the house of David—like God, like the messenger of Yahweh, before them.
Katika siku hiyo, Bwana atawakinga wale waishio Yerusalemu, ili kwamba aliye dhaifu kupita wote miongoni mwao awe kama Daudi, nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama Malaika wa Bwana akiwatangulia.
9 And it shall come to pass, in that day, —That I will seek to destroy all the nations, that come against Jerusalem.
Katika siku hiyo nitatoka kuangamiza mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu.
10 But I will pour out upon the house of David and upon the inhabitant of Jerusalem, the spirit of favour, and of supplications, and they will look unto me, whom they have pierced, —and will wail over him, as one waileth over an only son, and will make bitter outcry over him, as one maketh bitter outcry over a firstborn.
“Nami nitamiminia nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu roho ya neema na maombi. Watanitazama mimi, yule waliyemchoma. Nao watamwombolezea kama mtu anayemwombolezea mwanawe wa pekee na kusikitika kwa uchungu kama anayemsikitikia mzaliwa wake wa kwanza wa kiume.
11 In that day, will the wailing, be great, in Jerusalem, as the wailing of Hadadrimmon, in the valley of Megiddon;
Katika siku hiyo kilio kitakuwa kikubwa Yerusalemu, kama kilio cha Hadad-Rimoni katika tambarare ya Megido.
12 So shall the land, wail, family by family, apart, —the family of the house of David apart, and their wives apart, the family of the house of Nathan apart, and their wives apart;
Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yake, nao wake zao peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi na wake zao, ukoo wa nyumba ya Nathani na wake zao,
13 The family of the house of Levi, apart, and their wives apart, the family of Shimei, apart, —and their wives apart:
ukoo wa nyumba ya Lawi na wake zao, ukoo wa Shimei na wake zao,
14 All the families that remain, family by family, apart, —and their wives, apart.
na koo zote zilizobaki na wake zao.