< Psalms 91 >

1 He that dwelleth in the secret place of the Most High, Under the shadow of the Almighty, will tarry,
Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2 Saying of Yahweh—My refuge and my fortress, My God, in whom I will trust.
Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 For, he, will rescue thee, From the snare of the fowler, From the destructive pestilence.
Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 With his pinion, will he cover thee, And, under his wings, shalt thou seek refuge, A shield and buckler, is his faithfulness.
Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 Thou shalt not be afraid, Of the dread of the night, Of the arrow that flieth by day;
Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 Of the pestilence that, in darkness, doth walk, Of the plague that layeth waste at noonday.
wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 There shall fall, at thy side, a thousand, Yea, myriads, at thy right hand, Unto thee, shall it not come nigh;
Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Save only, with thine own eyes, shalt thou discern, And, the recompense of the lawless, shalt thou see.
Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 Because, thou, [hast made] Yahweh, my refuge, —The Most High, thou hast made thy dwelling-place,
Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 There shall not be sent unto thee misfortune, Nor shall, plague, come near into thy tent;
Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 For, his messengers, will he charge concerning thee, To keep thee, in all thy ways;
Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 On hands, will they bear thee up, Lest thou strike, against a stone, thy foot;
Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 On the lion and adder, shalt thou tread, Shalt trample on young lion and crocodile.
Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 Because, on me, he hath set firm his love, Therefore will I deliver him, I will set him on high, Because he hath known my Name;
Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
15 He shall call me, and I will answer him, With him, will, I, be, in distress, I will rescue him, and will honour him;
Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
16 With length of days, will I satisfy him, And will show him my salvation.
Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.

< Psalms 91 >