< Psalms 80 >

1 To the Chief Musician. For "the Lilies of Testimony." Asaph’s. A Melody. O Shepherd of Israel, give ear, Thou who leddest forth Joseph like a rock, Thou who art throned on the cherubim, appear!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Before Ephraim and Benjamin and Manasseh, stir up thy strength, And come! to our salvation.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 O God, bring us back, And light up thy face, That we may be saved.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 O Yahweh, God of hosts! How long hast thou been wroth with the prayer of thy people?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Thou hast fed them with the food of tears, And hast caused them to drink the water of weeping in threefold abundance.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Thou dost make us an object of contention to our neighbours, And, our foes, find mockery for themselves.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 O God of hosts, bring us back, And light up thy face, That we may be saved.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 A vine out of Egypt, thou didst remove, Thou didst cast out nations, and plant it;
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Thou didst make a clear space before it, So it rooted well its roots, and filled up the land;
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Covered were the mountains with its shade, And, with its boughs, the mighty cedars.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 It thrust forth its branches as far as the sea, —And, unto the River, its shoots.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Wherefore hast thou broken down its fences, So that all who pass along the way, pluck its fruit?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 The boar out of the forest, browseth upon it, And, the wild beast of the field, pastureth thereon.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 O God of hosts, return, we pray thee, —Look down out of the heavens, and see, And inspect this vine:
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 Yea the stock which thy right hand planted, Even upon the son thou didst secure for thyself.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 To be burned with fire, it is cut down, —At the rebuke of thy countenance, they will perish.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Let thy hand be, Upon the Man of thy right hand, Upon the Son of Man thou didst secure for thyself;
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 So will we not draw back from thee, Thou wilt bring us to life, And, on thy Name, will we call.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 O Yahweh, God of hosts! bring us back, Light up thy face, That we may be saved.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psalms 80 >