< Psalms 71 >

1 In thee, O Yahweh, have I sought refuge, May I not be ashamed unto times age-abiding:
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 In thy righteousness, wilt thou rescue me, and deliver me, Incline unto me thine ear, and save me:
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Be thou unto me, a Rock to dwell in, a Place of Security, To save me, For, my mountain crag and my stronghold, thou art.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Oh my God, deliver me, From the hand of the lawless one, From the clutch of the perverse and ruthless one;
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 For, thou, art my hope, My Lord, Yahweh, My confidence from my youthful days:
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 Upon thee, have I stayed myself from birth, Thou art he that severed me, from the body of my mother, Of thee, shall be my praise—continually.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 A very wonder, have I been unto many, Seeing that, thou, hast been my strong refuge,
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 My mouth shall be filled with, thy praise, All the day, with thy splendour.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 Do not cast me off in the time of old age, When my vigour faileth, do not forsake me;
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 For mine enemies have spoken of me, And, they who watch for my life, have taken counsel together;
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Saying, God, hath forsaken him, Pursue and take him, For there is none to rescue.
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 O God, be not far from me, O my God, to help me, make haste!
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Let them be ashamed—be consumed, Who are assailing my life, —Let them be covered with reproach and confusion, Who are seeking my hurt.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 But, I, continually will hope, And will add to all thy praise;
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 My mouth, shall relate thy righteousness, All the day, thy deliverance, For I know not the numbers.
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 I will enter into the mighty doings of My Lord—Yahweh, I will make mention of thy righteousness—thine alone.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 O God, thou hast taught me from my youthful days, And, hitherto, have I been wont to tell of thy wonders;
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Even now, therefore, that I am old and grayheaded, O God, do not forsake me, —Until I tell of thine arm unto a [new] generation, Unto every one that is to come, thy might;
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 And, as for thy righteousness, O God, up on high, Wherein thou hast wrought great things, O God! who is like unto thee?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Thou who hast let us see many distresses and misfortunes, Wilt again bring us to life, And, out of the resounding depths of the earth, wilt again raise us up;
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Thou wilt increase my greatness, And, on every side, wilt comfort me.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 I also, will praise thee by the aid of a harp, Thy faithfulness, O my God, —I will make music unto thee with a lyre, Thou holy one of Israel;
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 My lips shall make a joyful noise, When I make music unto thee, And my soul which thou hast ransomed;
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 Even my tongue, all the day, shall softly utter thy righteousness, For they have turned pale—for they have blushed, Who were seeking my hurt.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.

< Psalms 71 >