< Psalms 63 >
1 A Melody of David. When he was in the Wilderness of Judah. O God, my GOD, thou art, Earnestly do I desire thee, —My soul thirsteth for thee, My flesh fainteth for thee, In a land—dry, and weary for want of water, —
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 In like manner as, in the sanctuary, I have had vision of thee, To behold thy power and thy glory.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Because better is thy lovingkindness than life, My lips, aloud shall praise thee!
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Thus, will I bless thee while I live, In thy Name, will I lift up mine outspread hands:
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 As with fatness and richness, shall my soul be satisfied, And, with joyfully shouting lips, shall my mouth utter praise.
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 Should I call thee to mind upon my couch, In the watches of the night, would I breathe soft speech of thee.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 For thou hast become a help unto me, —And, in the shadow of thy wings, will I shout for joy.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 My soul hath run clinging to thee, On me, hath thy right hand laid hold.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 When, they, to crush it, would seek my life, They shall go into the lower parts of the earth:
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Every one shall be given up into the power of the sword, The portion of jackals, shall they become.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But, the king, shall rejoice in God, —Every one shall glory who sweareth by him, For the mouth of them who speak falsehood, shall be stopped.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.