< Psalms 6 >
1 To the Chief Musician, with stringed Instruments upon the eighth. A Melody of David. O Yahweh! do not, in thine anger, correct me, nor, in thy wrath, chastise me.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Show me favour, O Yahweh, for languishing am I: Heal me, O Yahweh, —for dismayed are my bones:
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 Yea, my soul, is dismayed greatly, Thou, then, O Yahweh—how long?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Return, O Yahweh, deliver my soul, Save me, for the sake of thy lovingkindness;
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 For, in death, is no remembrance of thee, —In hades, who shall give thanks unto thee? (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 I am weary with my sighing, I flood, through the whole night, my couch, —With my tears, I cause, my bed, to dissolve:
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 My face, is all sunken with sorrow, —it hath aged, because of all mine adversaries.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Depart from me, all ye workers of iniquity, for Yahweh hath heard the voice of my weeping:
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 Yahweh, hath heard my supplication, Yahweh, will receive, my prayer.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Let all my foes, turn pale and be greatly dismayed, Again let them turn pale in a moment.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.