< Psalms 49 >

1 To the Chief Musician. For the Sons of Korah. A Melody. Hear ye, this all ye peoples, Give ear, all ye inhabitants of this passing world;
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Both sons of the low, And sons of the high, —Together both rich and needy: —
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 My mouth, shall speak forth Wisdom, And the soft utterance of my heart be Understanding:
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 I will bend, to a by-word, mine ear, I will open, on the lyre, mine enigma.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Wherefore should I fear in the days of calamity, Though the iniquity of them who lie in wait for me should enclose me?
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 As for them who are trusting in their wealth, —And, in the abundance of their riches, do boast themselves,
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 A brother, can none of them, redeem, he cannot give unto God a ransom for himself:
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 So costly, is the redemption of their soul, That it faileth unto times age-abiding;
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 That he should, yet, live on, continually, Should not see corruption.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 For it is seen that, the wise, die, Together with the dullard, and the brutish, do they perish, And leave, to others, their wealth:
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 Their, inward thought, is that their houses are for times age-abiding, Their habitations, for generation after generation, —They give their own names unto lands!
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 But, a son of earth, though wealthy, cannot tarry, He hath made himself a by-word—Beasts, they resemble:
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 This, their way, is a folly to them, And yet, their followers, with their mouth, approve. (Selah)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Like sheep—into hades, are they driven, Death shall shepherd them, —And the upright shall have dominion over them in the morning, Even their form, is to decay, Hades, is all that remaineth of a habitation for him. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 But, God, will redeem my soul, out of the hand of hades, For he will take me. (Selah) (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 Do not fear, When a man becometh rich, When the glory of his house increaseth;
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 For, when he dieth, he shall take, nothing, his glory shall not descend after him;
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 For, though, his own self—while he lived, he used to bless, And they will praise thee, when thou doest well to thyself,
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 He shall enter as far as the circle of his fathers, Nevermore, shall they see the light.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 A son of earth though wealthy, who discerneth not, Hath made himself a by-word, Beasts, they resemble.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Psalms 49 >