< Psalms 48 >
1 A Melodious Song. For the Sons of Korah. Great is Yahweh, and worthy to be mightily praised, In the city of our God, His holy mountain.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in elevation, the joy of all the land, Is Mount Zion, in the recesses of the north, —The city of a great king.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 God, in her palaces, is to be known as a high tower.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 For lo! Kings—Met as appointed, Passed by together;
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 They themselves, saw, So, were they amazed, Dismayed—they hurried way!
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Trembling, seized them, there, Pangs. like hers who is in travail.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 With an east wind, wilt thou shatter the ships of Tarshish.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Just as we have heard, So, have we seen, In the city of Yahweh of hosts, In the city of our God, God himself, will establish her, unto times age-abiding. (Selah)
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 We have thought, O God, upon thy lovingkindness, In the midst of thy temple:
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 According to thy Name, O God, So, be thy praise, unto the ends of the earth, With righteousness, is, thy right hand, filled.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Let Mount Zion rejoice, Let the daughters of Judah exult, Because of thy judgments.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Go round Zion, and compass her about, Reckon up her towers;
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Apply your mind to her rampart, Pass between her palaces, That ye may recount them to an after generation;
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 For, this God, is our God, to times age-abiding and beyond, He himself, will conduct us till death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.