< Psalms 42 >

1 To the Chief Musician. An Instructive Psalm for the Sons of Korah. As, the hart, cometh panting up to the channels of water, So my soul, panteth for thee, O God.
Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
2 My soul thirsteth for God, for a GOD who liveth, —When shall I enter in, and see the face of God?
Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
3 My tears have been my food day and night, While it hath been said unto me all the day, Where is thy God?
Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
4 These things, I keep calling to mind, and pouring out, over me, my own soul, For I used to cross over with a crowd, Lead them in procession up to the house of God, With the voice of shouting and praise.—a throng keeping festival.
Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
5 Why shouldst thou be cast down, O my soul? And [why] shouldst thou moan over me? Wait thou for God, for yet shall I praise him, As the triumph of my presence.
Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
6 My God! over myself, my soul is cast down, —For this cause, will I remember thee from the land of Jordan, And the Hermons, from the hill Mizar.
Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
7 Roaring deep unto roaring deep, is calling, at the voice of thy cataracts, All thy breakers and thy rolling waves, over me, have passed.
Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
8 By day, will Yahweh command his lovingkindness, And, in the night, shall His song be with me, My prayer be to the GOD of my life.
Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
9 I will say onto GOD, —my rock, Wherefore hast thou forgotten me? Wherefore in gloom should I go, because of oppression by the enemy?
Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
10 With a crushing of my bones, have my adversaries reproached me, —While they keep saying unto me all the day, Where is thy God?
Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
11 Why shouldst thou be sat down, O my soul? And why shouldst thou moan over me? Wait thou for God, for yet shall I praise him, As the triumph of my presence and my God.
Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.

< Psalms 42 >