< Psalms 26 >
1 David’s. Do me justice, O Yahweh, For, I, in my blamelessness, have walked, and, in Yahweh, have I trusted, I will not waver.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Try me, O Yahweh, and prove me, Test my reins and my heart: —
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 For, thy lovingkindness, hath been before mine eyes, and I have walked to and fro in thy faithfulness;
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 I have not sat with men of deceit, nor, with dissemblers, would I enter;
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 I have hated the convocation of evil-doers, and, with lawless men, would I not sit;
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 I will bathe, in pureness, my hands, —so will I go in procession around thine altar, O Yahweh;
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 To sound aloud a song, and to recount all thy wonderful doings.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 O Yahweh, I have loved the asylum of thy house, even the place of the habitation of thy glory!
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 Do not remove, with sinners, my soul, nor, with men of bloodshed, my life;
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 In whose hands is a plot, and, their right hand, is filled with a bribe.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 But, I, in my blamelessness, will walk, Redeem me and show me favour.
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 My foot standeth in a level place, In the convocations, will I bless Yahweh.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.