< Psalms 146 >
1 Praise ye Yah, Praise, O my soul, Yahweh.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 I will praise Yahweh while I live! I will make melody to my God while I continue!
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 Do not ye trust in nobles, in a son of man who hath no deliverance:
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 His spirit, goeth forth, he returneth to his ground, In that very day, his thoughts perish.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 How happy is he that hath the GOD of Jacob as his help, whose hope, is on Yahweh his God: —
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 Who made The heavens and the earth, The sea and all that is therein, Who keepeth faithfulness to times age-abiding:
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 Who executeth justice for the oppressed, who giveth food to the famishing, Yahweh, who liberateth prisoners;
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 Yahweh, who opened [the eyes of] the blind, Yahweh, who raiseth the prostrate, Yahweh, who loveth the righteous;
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 Yahweh, who preserveth sojourners, The fatherless and widows, he relieveth, —but, the way of the lawless, he overturneth.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 Yahweh, will reign, to times age-abiding, Thy God, O Zion, to generation after generation. Praise ye Yah!
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.