< Psalms 137 >

1 By the rivers of Babylon, there, we sat down, yea we wept—when we remembered Zion:
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 Upon the willows—in the midst thereof, hanged we our lyres:
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 For, there, our captors asked of us words of song, and our plunderers—gladness, —Sing us of the songs of Zion!
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 How shall we sing the song of Yahweh, on a foreign soil?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 If I forget thee, O Jerusalem, Let my right-hand forget:
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 Let my tongue cleave to the roof of my mouth, if I do not remember thee! if I do not lift up Jerusalem above the head of mine own gladness.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Remember, O Yahweh, against the sons of Edom, the day of Jerusalem, —how they continued to say—Overthrow! Overthrow! unto the foundation within it.
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 O ruined daughter of Babylon, —how happy the man who shall repay thee thy dealing, wherewith thou didst deal with us!
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 How happy the man who shall snatch away and dash thy children against the crag.
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.

< Psalms 137 >