< Psalms 112 >
1 Praise ye Yah! How happy is the man who revereth Yahweh, In his commandments, delighteth he greatly;
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Mighty in the earth, shall be his seed, The generation of the upright, shall be blessed;
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Wealth and riches, shall be in his house, and, his righteousness, standeth for aye.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 Risen—in darkness, is light to the upright, The gracious and compassionate and righteous.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 Well for a man showing favour and lending! He shall sustain his affairs with justice.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 Surely, unto times age-abiding, shall he not be shaken, In remembrance, age-abiding, shall the righteous one remain;
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Of evil tidings, shall he not be afraid, Established is his heart, led to trust in Yahweh;
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 Upheld is his heart, he shall not be afraid, until that he gazeth on his foes.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 He hath scattered abroad, he hath given to the needy, His righteousness, standeth for aye, His horn, shall be exalted in honour.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 The lawless one, shall see, and be indignant, his teeth, will he gnash and melt away, The craving of the lawless, shall vanish.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.