< Proverbs 27 >

1 Do not boast thyself of to-morrow, for thou knowest not what a day may bring forth.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
2 Let another praise thee, and not thine own mouth, a stranger, and not thine own lips.
Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
3 Heavy is a stone, and weighty is sand, —but, the vexation of a fool, is heavier than both.
Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
4 The cruelty of rage, and the overflow of anger! But who can stand before, jealousy?
Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
5 Better is a rebuke that is open, than love carefully concealed.
Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
6 Faithful are the wounds of a friend, but lavished are the kisses of an enemy.
Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
7 The surfeited soul, trampleth upon droppings from the comb, but, to the hungry soul, every bitter thing, is sweet.
Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
8 As a bird wandering from her nest, so, is a man wandering from his place.
Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
9 Oil and perfume, rejoice the heart, the sweetness of one’s friend, more than fragrant wood.
Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
10 Thine own friend and thy father’s friend, do not thou forsake; but, the house of thy brother, do not enter, in thy day of calamity, Better a neighbour near, than a brother far off.
Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
11 Be wise, my son, and rejoice my heart, that I may answer him that reproacheth me in a matter.
Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
12 A prudent man, seeth calamity—he hideth himself, the simple, pass on—they suffer.
Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
13 Take a man’s garment when he hath become pledge for a stranger, then, for a female unknown, accept him as surety.
vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14 He that blesseth his friend, with a loud voice, in the morning early, a reproach, shall it be reckoned to him.
Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15 A continuous dripping on a day of downpour, and a contentious wife, are alike:
Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16 He that hideth her, hideth the wind, and, perfume, his right hand may proclaim.
kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17 Let, iron, by iron, become sharp, and let, a man, sharpen the face of his friend.
Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18 He that guardeth the fig-tree, shall eat the fruit thereof, and, he that watcheth over his master, shall be honoured.
Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19 As in water, face [answereth] to face, so, the heart of man to man.
Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20 Hades and destruction, are not satisfied, and, the eyes of a man, are not satisfied. (Sheol h7585)
Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
21 Fining pot for silver, and crucible for gold, and, a man, [is to be tried] by what he praiseth.
Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22 Though thou pound a fool in a mortar, amidst grain, with a pestle, his folly, will not depart from him.
Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23 Note well, the appearance of thy flock, apply thy mind to thy herds;
Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24 For, not age-abiding, are riches, nor is the diadem, from generation to generation: —
maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
25 The grass, is taken away, and the young shoot, showeth itself, and the herbage of the mountains, is gathered;
Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
26 There are, lambs, for thy clothing, and, for the price of thy field, there are he-goats;
Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
27 With, enough goats-milk, for thy food—for the food of thy household, and, a maintenance, for thy maidens.
Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.

< Proverbs 27 >