< Numbers 13 >
1 Then spake Yahweh unto Moses, saying:
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
2 Send for thee men and let them spy out the land of Canaan, which I am giving unto the sons of Israel, —one man each for the tribe of his fathers, shalt thou send, each one a prince among them.
Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
3 So then Moses sent them out of the desert of Paran, at the bidding of Yahweh, —all of them, great men, heads of the sons of Israel, were they.
Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
4 And, these, are their names, —Of the tribe of Reuben, Shammua, son of Zaccur;
Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Of the tribe of Simeon, Shaphat, son of Hori;
Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Of the tribe of Judah, Caleb, son of Jephunneh;
Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Of the tribe of Issachar, Igal, son of Joseph;
Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 Of the tribe of Ephraim, Hoshea, son of Nun;
Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Of the tribe of Benjamin, Palti, son of Raphu;
Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 Of the tribe of Zebulun, Gaddiel, son of Sodi;
kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 Of the tribe of Joseph—of the tribe of Manasseh, Gaddi son of Susi;
kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 Of the tribe of Dan, Ammiel, son of Gemalli;
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 Of the tribe of Asher, Sethur, son of Michael;
kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 Of the tribe of Naphtali, Nahbi, son of Vophsi;
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 Of the tribe of Gad, Geuel, son of Machi.
kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 These, are the names of the men, whom Moses sent to spy out the land, —but Moses called Hoshea son of Nun, Joshua.
Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17 So Moses sent them, to spy out the land of Canaan, —and said unto them—Go up, here in the South, Yea ye shall go up the mountain;
Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18 And shall see the land, what it is, —And the people that dwell thereupon, Whether they are, strong, or weak, Whether they are, few or many;
Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19 And what, the land, is, wherein they dwell, Whether it is, good, or, bad, —And the cities within which they dwell, Whether in camps or in strongholds;
Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20 And what the land is, Whether, fat, or, lean, Whether there is timber therein or is not, Then shall ye pluck up courage and take of the fruit of the land. Now the days, were the days of the first-fruits of grapes.
Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
21 So they went up, and spied out the land, —from the wilderness of Zin unto Rehob at the entering in of Hamath.
Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
22 Yea they went up in the South and entered as far as Hebron, and there, were Ahiman Sheshai and Talmai descendants of the Anak. Now, Hebron, was built seven years, before Zoan of Egypt.
Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
23 And they entered as far as the ravine of Eschol, and cut down, from thence a branch with one cluster of grapes, and bare it on a pole between two, —also of the pomegranates and of the figs.
Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
24 That place, was called, The Ravine of Eschol ["Cluster-ravine"]—on account of the cluster, which was cut down from thence by the sons of Israel.
Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
25 And they returned from spying out the land, —at the end of forty days.
Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 So they took their journey, and came in unto Moses and unto Aaron and unto all the assembly of the sons of Israel into the wilderness of Paran, towards Kadesh, —and brought back word—unto them and unto all the assembly, and showed them the fruit of the land.
Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
27 And they recounted unto him, and said, We entered into the land whither thou didst send us, and surely it doth flow with milk and honey, and, this, is the fruit thereof.
Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
28 Nevertheless surely mighty, are the people that dwell in the land, —and, the cities, walled in, exceeding great, moreover also, the descendants of the Anak, saw we there.
Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
29 Amalek, dwelleth in the land of the South; And, the Hittite, and the Jebusite and the Amorite, dwell in the mountain And the Canaanite, dwelleth by the sea, and by the side of the Jordan.
Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
30 And Caleb stilled the people unto Moses, —and said unto them—Let us go straight up, and possess it, for we shall, surely prevail, against it.
Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
31 But the men who went up with him said, We cannot go up against the people, —for stronger, are they than we.
Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
32 So they sent forth a rumour of the land which they had spied out, among the sons of Israel, saying, —As touching the land through which we passed to spy it out, it is, land that eateth up them who dwell therein, And all the people that we saw in the midst thereof, were men of great stature.
Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
33 And, there, saw we the giants, sons of Anak [descended] of the giants, —And we were in our own eyes, as grass-hoppers, And, so, were we in their eyes.
Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”